Monday, July 2, 2012

Wanafunzi wasema kuuza Rambo kunalipa sio shule.........

BAADHI ya watoto wanaostahili kwenda shuleni kuhudhuria masomo, wamekuwa ni kero kwenye masoko mbalimbali jijini Arusha kutokana na kuuza mifuko ya plastiki maarufu Rambo.

Aidha, watoto hao wamedai uuzaji wa rambo hizo kunalipa zaidi badala ya kuhudhuria masomo yasiyo na manufaa kwao na wengine wanalinda magari ya wananchi wanaofika sokoni kununua mahitaji yao.

Mwandishi wa habari hii alitemb
elea soko la Kilombero na Soko Kuu na kukuta watoto hao wanaostahili kwenda shule nyakati za asubuhi wakikimbilia wateja na kuwauzia mifuko ya Rambo kwa Sh 100 kisha kung’ang’ania kubea mizigo isiyoendana na uzito/umri waliokuwa nao.

Mmoja kati ya watoto hao, Emmanuel Joel (11) alisema anasoma darasa la tatu katika shule ambayo hakutaka kuitaja, lakini kutokana na mazoea ya kuuza mifuko hiyo na kupata faida zaidi, ameona shuleni hatapata maendeleo na kuamua kujikita kwenye biashara hiyo ili apate fedha za kujikimu.

Alisema familia yao sio duni, lakini anauza mifuko hiyo kutokana na kupata fedha na asubuhi anavaa nguo za shule na kwenda shule, lakini akifika eneo fulani anajificha kisha anabadili nguo na kwenda sokoni kuuza mifuko hiyo na muda wa kurudi shule ukifika anakwenda nyumbani kama kawaida.

“Mazaa hii kazi inalipa kuliko masomo hivyo nimeona bora niifanye ili nipate fedha nikiuza mifuko yote napata faida ya shilingi elfu mbili au elfu mia tano kwa siku na nikibeba mizigo, bei ni maelewano kati yangu na mwenye mizigo hivyo ndio maisha kwani sioni sababu ya kusoma wakati napata fedha,” alidai.

Hata hivyo, jitihada za Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Arusha, Estomih Chang’a za kutoa matangazo yanayowataka watu wazima kutoajiri watoto au kununua Rambo zinazouzwa na watoto hao, zimegonga mwamba kutokana na watoto hao kufanya biashara kama kawaida ingawa matangazo wanayasikia.

No comments:

Post a Comment