Saturday, November 17, 2012
Kumbe Hii Ndio Sababu ya Hussein Machozi kuhamia Kenya
Msanii mahiri wa Bongo Fleva almaarufu kama Hussein Machozi baada ya kutamba na ngoma zake kadhaa kali kama Addicted,Mizimu,Kwa ajili yako na ngoma zingine kali sasa Latest info kutoka kwa msanii huyu ni kwamba baada ya kufanya ngoma ya mpya ambayo ilikuwa inakwenda kwa jina la Addicted huko kenya sasa ameamua kufunguka na kuweka wazi sababu ambazo zimemfanya mpaka aanze kufanya kazi zake nchini kenya,alieleza kwamba kwanza nchini Kenya kwa wiki anapata show mara tatu pia kule muziki wake unalipa sana kushinda huku bongo na ndiyo maana ameamua kufanya kazi zake nchini kenya
Sunday, November 4, 2012
THE BEST AGE TO BE SINGLE AND DATING.......
The single best decade for dating is...
Think it’s scary and miserable to be an older dater? Think again.
Conventional wisdom holds that dating success and enjoyment are like the contents of a milk carton, because they come with an expiration date. But recent research indicates that older daters are also the happiest daters — a surprise, no doubt, to those in their twenties who think that romance is solely for the young. As it turns out, the “young at heart” have it going on much more than anyone previously realized.
According to a recent study from Match.com, older singles report feeling the greatest level of happiness combined with the least amount of stress over their relationship status. So, you can relax about being single and/or dating after a certain age, because your love life down the road could be much better than you expect. Of course, that’s not to say that people in different age groups want the same things in a match; after all, everyone’s life stages are distinct, and what we want and need at 20 differs radically (for the most part) from what we want when we’re 60.If you need to be single you can Browse Local Singles at Match.com on Yahoo!
UJANA MAJI YA MOTO....BE SINGLE.......FANYA MAMBO YAKO JIJENGE THEN BE IN DATING......WAZURI HAWAISHIIII
Think it’s scary and miserable to be an older dater? Think again.
Conventional wisdom holds that dating success and enjoyment are like the contents of a milk carton, because they come with an expiration date. But recent research indicates that older daters are also the happiest daters — a surprise, no doubt, to those in their twenties who think that romance is solely for the young. As it turns out, the “young at heart” have it going on much more than anyone previously realized.
According to a recent study from Match.com, older singles report feeling the greatest level of happiness combined with the least amount of stress over their relationship status. So, you can relax about being single and/or dating after a certain age, because your love life down the road could be much better than you expect. Of course, that’s not to say that people in different age groups want the same things in a match; after all, everyone’s life stages are distinct, and what we want and need at 20 differs radically (for the most part) from what we want when we’re 60.If you need to be single you can Browse Local Singles at Match.com on Yahoo!
UJANA MAJI YA MOTO....BE SINGLE.......FANYA MAMBO YAKO JIJENGE THEN BE IN DATING......WAZURI HAWAISHIIII
Tuesday, October 23, 2012
F.D.A. Receives Death Reports Citing Popular Energy Drink.....
Five people may have died in recent years after drinking Monster Energy, a popular energy drink that is high in caffeine, according to incident reports recently released by the Food and Drug Administration.
The reports, like similar filings made with the F.D.A. in cases connected with drugs or medical devices, do not prove a link between Monster Energy and the deaths or health problems. The records were recently obtained under the Freedom of Information Act by the mother of a 14-year-old Maryland girl who died in December from a heart arrhythmia after drinking large cans of Monster Energy on two consecutive days.Last week, Wendy Crossland, the mother of that teenager, filed a lawsuit against Monster Beverages, a publicly traded company in Corona, Calif., that used to be known as Hansen Natural. The lawsuit charges that Monster failed to warn about the risks of its energy drinks; a spokeswoman for the company said last week that its products were safe and not the cause of the teenager’s death.
That spokeswoman, Judy Lin Sfetcu, added that Monster was “unaware of any fatality anywhere that has been caused by its drinks.”
In an interview, an F.D.A. spokeswoman, Shelly Burgess, said the agency had received reports of five deaths possibly linked to the drink as well as another report of a heart attack. The reports cover a period of 2004 to June of this year.
The reports do not make clear whether the incidents involved other factors, like alcohol or drugs. However, the number of reports that the F.D.A. receives about any product it regulates usually understates by a large degree the actual number of problems.
The release of the filings about Monster Energy may increase Congressional calls for greater regulation of the energy products industry. Monster Energy is among scores of energy drinks like Red Bull and Rock Star, and energy “shots” like 5-hour Energy, that companies are aggressively marketing to teenagers and young people.
In a statement, Ms. Burgess, the F.D. A. spokeswoman, said that it was the responsibility of energy drink manufacturers to investigate accusations of death or injuries associated with them. She said that the agency was still looking into the cases but had yet to establish a causal link between the deaths and the drink.
Monster Beverage makes a variety of energy drinks with names like Monster Rehab, Monster Assault and Monster Heavy Metal. Labels on the containers state that they are “not recommended” for some consumers, including children — a group that beverage producers define as those under 12 years — and people “sensitive” to caffeine.
Monster Energy did not immediately respond Monday to a request for comment on the F.D.A. filings.
Under current F.D.A. rules, companies do not need to disclose caffeine levels in their beverages and can choose to market them as drinks or as dietary supplements. Those various regulatory categories have differing labeling and ingredient rules.
While healthy adults can consume large quantities of caffeine from sources like coffee, tea and energy drinks, the drug, which acts as a stimulant, can pose risks to those with underlying conditions like heart disorders.
The type of 24-ounce can of Monster Energy that the Maryland teenager, Anais Fournier, drank contains 240 milligrams of caffeine, three times the amount found in an 8-ounce can of Red Bull and about 50 milligrams more than in the 20-ounce size of Red Bull.
The lawsuit filed last week on behalf of the teenager referred to autopsy and medical examiner reports that said she had died of “cardiac arrhythmia due to caffeine toxicity” that had exacerbated an existing heart problem.
A lawyer for her family, Kevin Goldberg, said that the 14-year-old had been aware she had an underlying condition but added that her doctors had not told her to restrict her physical activities or her caffeine use.
In an April letter citing the teenager’s death, Senator Richard J. Durbin, Democrat of Illinois, urged the F.D.A. to enforce caffeine levels in energy drinks.
In August, F.D.A. officials responded by saying that there was insufficient evidence to take action on caffeine levels in energy drinks. However, the agency also noted then that it had not yet received medical reports related to the Maryland teenager’s death.By BARRY MEIER | New York Times – 13 hours ago powered by MALETHO SON...BLOGSPOT.
Monday, October 22, 2012
AM BACK NOW TO KEEP YOU UPDATE........MA FANS!!!!
i waz biz wit working staffs visafari vya hapa na pale but nw am back i knw you mis me ma news,informative and otherz....but all in all am back.....get ready for hot newz......yereeeeeeeeeee!
Pembe za ndovu kutoka Dar zanaswa Hong Kong......
MAOFISA Forodha wa Hong Kong wamekamata kontena mbili za pembe za ndovu zenye thamani Dola za Marekani 3.4 milioni (wastani wa Sh5.4 bilioni), zinazodaiwa kupelekwa huko zikitokea Tanzania na Kenya.
Pembe hizo, vipande 1,209 vyenye uzito wa tani nne, zilikamatwa juzi nchini humo zikiwa kwenye kontena mbili ambazo ziliwekwa alama kuwa zimebeba plastiki chakavu na maharagwe aina ya roscoco.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na gazeti dada la Mwananchi (The Citizen), alisema amepata taarifa za kukamatwa kwa pembe hizo na atatoa maelezo baadaye.
“Nimepata taarifa, lakini siwezi kuzungumzia hilo sasa hivi kwa kuwa tuko katika mchakato wa kuuza akiba ya pembe za ndovu tulizonazo.”
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Paul Sarakikya alisema hana taarifa kuhusu kukamatwa kwa pembe hizo na kuahidi kufuatilia.
“Hatujapata hizo taarifa, kwani wewe umezipata wapi? Gazeti gani hapa Tanzania limeandika habari hizo! Kama hazijaandikwa, ndiyo kwanza wewe unanipa taarifa, hivyo tutafuatilia,” alisema na kuongeza kuwa watawasiliana na Idara ya Polisi wa Kimataifa (Interpol), ili waweze kujua undani wa suala hilo.
Taarifa kutoka Hong Kong zinasema hiyo ni mara ya kwanza kwa kiasi kikubwa kama hicho cha pembe za ndovu kukamatwa nchini humo zikiwa zimefichwa ndani ya mabegi yaliyokuwa na plastiki chakavu pamoja na maharagwe.
Kugundulika kwa pembe hizo imeelezwa kulitokana na taarifa zilizotolewa na maofisa wa Serikali ya China kwa maofisa forodha wa Hong Kong.
Kutokana na tukio hilo, Serikali ya China imewakamata watu saba akiwamo mkazi mmoja wa Hong Kong kuhusiana na pembe hizo.
Kukamatwa kwa pembe hizo kumekuja wakati Serikali ikiwa imeomba upya kwa Umoja wa Mataifa, kuuza akiba yake ya pembe za ndovu zilizotaifishwa ili kupata fedha za kuimarisha ulinzi, kwa lengo la kumaliza tatizo la ujangili.
Ripoti zinaeleza kuwa idadi ya tembo katika Bara la Afrika imepungua kutoka mamilioni katikati ya karne ya 20 hadi kufikia 600,000 mwishoni mwa miaka ya 1980.
Biashara haramu ya pembe za ndovu imetokana na mahitaji makubwa kutoka Bara la Asia na nchi za Mashariki ya Kati, ikidaiwa kuwa hutumika kutengeneza dawa za asili. Bara la Afrika linakadiriwa kuwa na tembo 472,000.
Pembe hizo, vipande 1,209 vyenye uzito wa tani nne, zilikamatwa juzi nchini humo zikiwa kwenye kontena mbili ambazo ziliwekwa alama kuwa zimebeba plastiki chakavu na maharagwe aina ya roscoco.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki akizungumza na gazeti dada la Mwananchi (The Citizen), alisema amepata taarifa za kukamatwa kwa pembe hizo na atatoa maelezo baadaye.
“Nimepata taarifa, lakini siwezi kuzungumzia hilo sasa hivi kwa kuwa tuko katika mchakato wa kuuza akiba ya pembe za ndovu tulizonazo.”
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Paul Sarakikya alisema hana taarifa kuhusu kukamatwa kwa pembe hizo na kuahidi kufuatilia.
“Hatujapata hizo taarifa, kwani wewe umezipata wapi? Gazeti gani hapa Tanzania limeandika habari hizo! Kama hazijaandikwa, ndiyo kwanza wewe unanipa taarifa, hivyo tutafuatilia,” alisema na kuongeza kuwa watawasiliana na Idara ya Polisi wa Kimataifa (Interpol), ili waweze kujua undani wa suala hilo.
Taarifa kutoka Hong Kong zinasema hiyo ni mara ya kwanza kwa kiasi kikubwa kama hicho cha pembe za ndovu kukamatwa nchini humo zikiwa zimefichwa ndani ya mabegi yaliyokuwa na plastiki chakavu pamoja na maharagwe.
Kugundulika kwa pembe hizo imeelezwa kulitokana na taarifa zilizotolewa na maofisa wa Serikali ya China kwa maofisa forodha wa Hong Kong.
Kutokana na tukio hilo, Serikali ya China imewakamata watu saba akiwamo mkazi mmoja wa Hong Kong kuhusiana na pembe hizo.
Kukamatwa kwa pembe hizo kumekuja wakati Serikali ikiwa imeomba upya kwa Umoja wa Mataifa, kuuza akiba yake ya pembe za ndovu zilizotaifishwa ili kupata fedha za kuimarisha ulinzi, kwa lengo la kumaliza tatizo la ujangili.
Ripoti zinaeleza kuwa idadi ya tembo katika Bara la Afrika imepungua kutoka mamilioni katikati ya karne ya 20 hadi kufikia 600,000 mwishoni mwa miaka ya 1980.
Biashara haramu ya pembe za ndovu imetokana na mahitaji makubwa kutoka Bara la Asia na nchi za Mashariki ya Kati, ikidaiwa kuwa hutumika kutengeneza dawa za asili. Bara la Afrika linakadiriwa kuwa na tembo 472,000.
Wednesday, September 12, 2012
IFWA part.......
APART WICH WILL BASE FOR SHARING IDES,FASHION,BIZNESS,SUPPORT,JOB SICKER AND OTHER MORE.its starter on 2012 by WAKUNGARAA C.O innocent maletho.The long term of word IFWA is INSIDE FIND WHAT U WANT(IFWA)so soon iwill open the link abt this for many people to login and share this is aim to an able youth to connect each other easy and for reason of develop ment put ur comment down then next time open the link iwill rich to another steps..KWAN WALE WANANN SS TUSHINDWE KWANNN???C YA
Saturday, August 25, 2012
Barack Obama Ana Kiwanda Cha Bia ndani ya White House......
Kuongoza nchi kubwa kama Marekani yataka moyo! Ndio maana Barack Obama aliamua kuwa na kiwanda cha bia kwenye ikulu ya White House ili kupunguza stress za cheo hicho kikubwa duniani. Isitoshe kipindi hiki ni kigumu kwake kwakuwa anaelekea kwenye uchaguzi, so kupiga mtungi si jambo la kushangaza kwake.
Amekuwa rais wa kwanza wa hivi karibuni nchini Marekani kunywa bia inayotengezwa kwenye Ikulu.
Bia inayotengenezwa humo imepewa jina la ‘White House Honey Ale’ ikiwa na rangi mbalimbali.
Asali kidogo inayopatikana kwenye bia hiyo inatoka kwenye mizinga ya nyuki anayofuga mkewe Michelle Obama kwenye bustani yao.............
Asali kidogo inayopatikana kwenye bia hiyo inatoka kwenye mizinga ya nyuki anayofuga mkewe Michelle Obama kwenye bustani yao.............
Facebook will disappear in the future....
Arcording to the expert's prediction, Facebook will be disappeared in next 5 to8 years . This information make the users in the internet tumult and worry in the recent weeks. However, the experts are not really shocked if it will happen reality.
Eric Jackson, founder of Ironfire Capital, said that in 5 to 8 years, Facebook will be disappeared in a way similar to Yahoo disappear. " Whether Yahoo is still making money, still profitable, still has 13 thousand employees working for them but they were only 10% in profit compared with their highest profit in 2000. That means unsuccessful and disappear
Jackson noted that, until this moment, the world has developed three generations of Internet companies. The first is Yahoo, a Web portal. This is a great example as a pioneer in the online field.Facebook then as the second generation with the wave of social media. The third generation is the world's mobile phone.
One of the problems for Facebook as the company can not make money from growing base of mobile phones. According to Jackson, Facebook will face challenges when moving into the mobile phone market like Google faced difficulties entering the field of social networks.
On the other side, predicted a collapse on Facebook comes just weeks after social networks have trouble with the IPO shares. Many financial analysts said that the company introduce the shares in the market was too high and it can never turn back to the first price.
Dan Olds, an analyst at consulting Gabriel Consulting Group agree with the views of Jackson, mobile phones will serve as increasingly important for any Internet company would, especially social networks . However, he believes too early to say Facebook will be thrown away of the mobile phone market.
Dan Olds said "Facebook is progressing slowly in the field of mobile phones. Most users see Facebook interface for mobile phone hardly to see. However, Facebook recently redesigned interface for mobile phones to view images more easily. But Facebook also needs to build a mobile business model so we can improve to attract advertisers.
Brad Shimmin, an analyst at CurrentAnalysis, agree with the view that, mobile phone is important, the foundation can help Facebook prosper and Facebook can also shield fall
Eric Jackson, founder of Ironfire Capital, said that in 5 to 8 years, Facebook will be disappeared in a way similar to Yahoo disappear. " Whether Yahoo is still making money, still profitable, still has 13 thousand employees working for them but they were only 10% in profit compared with their highest profit in 2000. That means unsuccessful and disappear
Jackson noted that, until this moment, the world has developed three generations of Internet companies. The first is Yahoo, a Web portal. This is a great example as a pioneer in the online field.Facebook then as the second generation with the wave of social media. The third generation is the world's mobile phone.
One of the problems for Facebook as the company can not make money from growing base of mobile phones. According to Jackson, Facebook will face challenges when moving into the mobile phone market like Google faced difficulties entering the field of social networks.
On the other side, predicted a collapse on Facebook comes just weeks after social networks have trouble with the IPO shares. Many financial analysts said that the company introduce the shares in the market was too high and it can never turn back to the first price.
Dan Olds, an analyst at consulting Gabriel Consulting Group agree with the views of Jackson, mobile phones will serve as increasingly important for any Internet company would, especially social networks . However, he believes too early to say Facebook will be thrown away of the mobile phone market.
Dan Olds said "Facebook is progressing slowly in the field of mobile phones. Most users see Facebook interface for mobile phone hardly to see. However, Facebook recently redesigned interface for mobile phones to view images more easily. But Facebook also needs to build a mobile business model so we can improve to attract advertisers.
Brad Shimmin, an analyst at CurrentAnalysis, agree with the view that, mobile phone is important, the foundation can help Facebook prosper and Facebook can also shield fall
Moshi Ufundi: Sekondari iliyogeuka kuwa magofu....(MOSH TECH)
HAINA CHOO, BAFU, WANAFUNZI WAJISAIDIA VICHAKANI.....
Kijana akipiga mswaki eneo la shule ya Sekondari ya Ufundi Moshi iliyopo Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro.
SHULE ya Sekondari ya Ufundi Moshi iliyopo Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro ni miongoni mwa shule za Serikali iliyokuwa ikifanya vizuri kwa kutoa wasomi wengi miongoni wapo serikalini na taasisi binafsi.
Ilianzishwa mwaka 1957 ikiwa kama shule ya masomo ya biashara na ilipofikia mwaka 1967 ilibadilishwa na kuwa shule ya sekondari ya ufundi kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne.
Kwenye miaka ya 1970 na 1980, ilikuwa na mazingira nadhifu kwa kuwa na majengo ya mabweni na vyumba vizuri vya kusomea. hali hiyo pia ilikuwa ikiandamana na matokeo mazuri kwa wanafunzi wengi.
Leo hii ukichunguza mazingira yake yalivyo ukalinganisha na hali na hadhi iliyokuwa nayo miaka 30 iliyopita waweza kupata wazo ambalo linawiana na msemo wa Kiswahili usemao: "Ngoma ikivuma sana mwisho wake hupasuka."
Sasa iko katika hali mbaya kiasi kwamba hata wanafunzi hawawezi kuingia msalani kutokana na miundombinu ya shule hiyo kuwa mibovu kupita kiasi.
Leo hii wanafunzi waalazimika kutumia choo kilichojenga mwaka juzi kwa ajili ya walemavu chenye matundu matatu ambacho kinatumiwa na wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha sita.
Mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo anasema vyoo na bafu vilijengwa tangu shule ilipoanzishwa na vimekuwa havifanyiwi ukarabati wala kujengwa vipya jambo ambalo limesababisha kuchakaa kiasi kwamba havifai kutumika.
Ukiingia baadhi utaona kuta zimoka sakavu imeharibika na vingi vinatiririsha maji machafu pembeni nu kusababisha vigeuke kuwa mazalia ya nzi, mende na wadudu wengine wanaotambaa.
Anasema wanafunzi wanashindwa kuvitumia vyoo hivyo mchana na mara nyingine wanajikuta wakilazimika kwenda kijisaidia kwenye vichaka karibu na shule hiyo.
Kutokuwa na maeneo ya kujisetiri faraga wakati wa kuoga, kumekuwa kukiwafanya wasubiri usiku wa giza ambao siyo rahisi kuonekana wao kwa wao au wapitanjia.
Alisema kufuatia uchakavu wa majengo, baadhi ya mabati yaliyoezekea majengo hayo yametoboka na wakati wa mvua yanavuja na hata kusababisha dari kuchakaa na mara kadhaa vipande vyake vimekuwa vikiwadondokea.
“Yaani hii shule iko katika hali mbaya kiasi kwamba hata sisi tunaosoma hapa tunaona tuko kama tunasomeshwa bure kumbe tunalipa ada na wazazi wanajua tuko katika shule nzuri. Kumbe mazingira haya ni mabaya," anasema mawafunzi huyo.
Uchakavu wa shule hiyo ipo hadi kwenye miundo mbinu ya usambazaji wa umeme na sasa majengo mengi hayana umeme jambo linalowalazimisha wanafunzi kutumia mishumaa wakati wa kusoma.
Licha ya uchakavu huo, wanafunzi wanalalamika kwamba wanafunzi wanaosajiliwa kila mwaka ni wengi kuliko uwezo wake.
“Kwa kweli! Kiwango cha elimu hapa shuleni kinashuka kutokana na mfumo wa shule ulivyo waalimu hawajali ni sawa na kwamba hawathamini kazi zao na mazingira wanayofanyia," anasema mmoja.
Anatoa mfano wa darasa lake kuwa lina wanafunsi zaidi ya 100 wakati uwezo wake halisi ni kati ya 45 hadi 50.
Anasema wakati mwalimu anafundisha, baadhi ya wanafunzi hushindwa kuingia darasani na kubakia kusikiliza wakiwa nje jambo ambalo linapunguza usikivu wa umakini.
“Wanafunzi wengi hawaingii darasani kwa kuwa unakuta hakuna sehemu ya kukaa wakiingia wengine wanakuwa wanazunguka tu na wala walimu hawasemi chochote,” analalamika mwanafunzi huyo.
Tatizo jingine ni shule hiyo kutokuwa na vifaa vya kufundishia wanafunzi walemavu, jambo ambalo linawapa shida kuendana na mazingira halisi ya ufundishaji hivyo kushindwa kupata elimu iliyokusudiwa.
Wanafunzi hao walisema walemavu walioko shuleni hapo hawatendewi haki kwa kuwa wanachanganywa na wanafunzi wakawaida bila kujali ni mlemavu wa aina gani.
“Hapa shuleni tuna walemavu ambao hawana uwezo wa kusikia sauti na wengine wasioona na vipofu na huwa tunachanganywa nao madarasani hawana waalimu wa kuwafundisha na unakuta hata hawaelewi chochote.” alisema.
Alisema baadhi ya waalimu hawaingii kufundisha darasani na pale wakijisikia na pale tunapohoji wanafunzi wanafukuzwa shule kwa kuwa hivi karibuni kuna baadhi ya viranja pamoja na wanafunzi ambao walihoji kuhusu ufundishaji na wote walifukuzwa.
Alisema wanafunzi wengi wamekuwa wanahofia kuzungumza hadharani matatizo ya shule hiyo kwa hofu ya kufukuzwa shule.
“Pamoja na ubovu wa vyoo, madarasa na mabafu hatuthubutu kulalamika kwa kuwa hofu ni kupatiwa barua ya kufukuzwa shule,” alilalamika.
Anadai kuna wanafunzi waliwahi kufukuzwa shule kutokana na kitendo cha kuhoji ratibu ya vyakula kwa sababu wanafunzi wamekuwa wakipikiwa Ugaki na maharage kila siku.
Anasema wanahofia maisha yao wakati wakiwa wamelala kutokana na bweni la wasichana kubomoka na wote kuhamia gorofa ya kwanza ambapo wanalazimika kulaa wanafunzi wanane hadi 10 katika chumba kimoja ambacho kina uwezo wa kulaza wanafunzi wanne.
Anaema gorofa ya juu ya jengo wanalolala limebomoka na hata ngazi zimevunjika kiasi kwamba ni hatari katika maisha yao.
“Tumelalamika kwenye uongozi wa mara kadhaa bila mafanikio,: lialaliachochote na ndio shule tuliopangiwa tukifikiria wengine wazazi wetu hawana uwezo wa kutuhamisha kwenda shle nyingine inatubidi tuvumilie shida hizi,” anasema.
Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo Maddy Kisuu, alikiri shule hiyo kukabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za uchakavu wa majengo, miundo mbinu na kushuka kiwango cha taaluma.
Kisuu anasema hali hiyo imechangiwa na Serikali kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na shule hiyo huko miundombinu ya majengo ikiwa ni ile ile.
Anasema shule hiyo yenye wanafunzi 1,476 ina waalimu 17 na kusababisha kiwango cha elimu kushuka kupita kiasi kutokana na upungufu wa walimu.
Mkuu huyo anasema shule hiyo pia ina wanafunzi wenye matatizo ya kusikia 100 lakini ina walimu 5 kwa ajili yao jambo ambalo halitoshelezi kukidhi matakwa yao kikamilifu.
Anasema shule hiyo ni miongoni mwa zile zilizokuwa zikitoa wataalamu mbalimbali wa ufundi nchini lakini kwa sasa kiwango cha elimu kimeshuka kutokana na kukoza mazoezi kwa vitendo.
Katika kuthitisha hilo, anasema rekodi ya matokeo ya mithani wa kidato cha nne mwake 2007 yanaonyesha wanafunzi waliofaulu kwa daraja la kwanza 60 kati wanafunzi 230. Katika mwaka 2009 wanafunzi 14 tu kati ya 117 ndio waliofauli daraja la kwanza na na mwaka 2011 wanafunzi 29 kati ya 153 ndio walofaulu kwa daraja la kwanza.
Kwa matokeo ya kidato cha sita 2006 /2007 wanafunzi saba kati ya 152 ndio walifaulu kwa daraja la kwanza na 2007 /2008 hakukua na aliyefaulu kwa daraja la kwanza kati ya wanafunzi 101 na mwaka 2010/2011
waliofaulu kwa daraja la kwanza walikuwa tisa kati ya 151 na 2011/2012 wanafunzi wawili kati ya 183 ndio walifaulu kwa daraja la kwanza.
Kwa upande wa walemavu, hakuna aliyeweza kufaulu kwa miaka mitatu mfululizo iliyopita.
Wednesday, August 8, 2012
WATOTO WA MITAANI WATISHIA USAFI MOSHI MJINI.....
HALMASHAURIA ya Manispaa ya Moshi inakabiliwa na ongezeko la watoto wa mitaani wanaotishia kuibuka kwa vitendo vya uhalifu, huku mashirika ya Serikali na yasio ya Serikali yakitakiwa kusaidia kutoa elimu na ajira.
Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita, Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Bernadette Kinaboalisema halmashauri ina hofu baada ya ongezekola watoto wa mitaani,hali inayoweza kusababisha kuongezeka kwa vitendo vya ujambazi na magonjwa ya maambukizi.
Kinabo alisema mwaka 2009 Manispaa ya Moshi ilikuwa na watoto wa mitaani 4,600, ambao walitoka familia za ndoa zilizovunjika ikiwamo umaskini uliowaondoa majumbani kwa kukosa huduma muhimu.
Alisema zaidi ya nusu watoto hao wanasomeshwa na taasisi zisizo za Serikali na wengine wanasomeshwa kupitia magari (Mobile School ), badala yake wamekuwa wakirejea mitaani na kujitumbukiza katika vitendo viovu na uporaji.
“Kwa kweli kila siku ziendavyo halmashauri inazidi kukabiliwa na ongezeko la watoto wa mitaani licha ya mji wetu kuwa msafi, wamekuwa wachafuzi wakubwa kwa baadhi ya maeneo,” alisema Kinabo.
Kuhusu usafi wa mji huo, Kinabo alisema tangu mwaka 2006 ilipoweka sheria ndogo ya usafi wa mazingira ikisaidiana na sheria ndogo ya ada na ushuru ya mwaka huohuo, wamekuwa na mafanikio makubwa wa kuuweka mji wa Moshi katika hali ya usafi wa hali ya juu.
Alisema mji huo umekuwa wa kwanza kwa usafi katika halmashauri 17 nchini kwa miaka mitano mfululizo, hivyo kuwafanya wageni wakiwamo watalii kutembelea mara kwa mara ikiwamo maeneo ya vivutio.
Alisema hali hiyo imesababisha kutoa ajira kwa vikundi vya jamii na kupata ufadhili kutoka mji wa Delray Beach, nchini Marekani na kwamba, karibu watawasili hivi karibuni kuimarisha vikundi kazi kupitia mradi wao wa Manispaa ya Moshi.
Saturday, August 4, 2012
Zitto atoa ya moyoni kuhusu madai ya rushwa........
WAKATI shinikizo la kuvunjwa kwa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC), kwa tuhuma za ufisadi likiendelea, Mwenyekiti wake, Zitto Kabwe ameibuka na kukituhumu chama tawala CCM, Serikali na baadhi ya wapinzani akidai kuwa wana uchu wa kuiongoza kamati hiyo na wanaratibu mkakati wa kumchafua.
Kwa sababu hiyo, amepinga maoni ya baadhi ya wabunge wanaotaka ivunjwe na badala yake akasema kama kuna ushahidi wa kutosha dhidi ya vitendo vya rushwa, basi awajibike yeye.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Zitto alisema licha ya mkakati huo, katu hatarudi nyuma katika kutetea masilahi ya taifa kwa kuwa anaamini siku zote uongo hujitenga na ukweli.
“Mchango wa POAC katika Bunge na ustawi wa mashirika ya umma ni bayana na haujawahi kutiliwa shaka. Kamati yetu imeokoa upotevu mkubwa wa mali na fedha za umma kutokana na umakini wake,” alisema Zitto na kuongeza:
“Tumefanya hivyo CHC, Kiwira na kwenye mashirika mengi. Kote huku uadilifu wa kamati hii haujawahi kuhojiwa. Zipo hoja pandikizi za kutaka POAC ivunjwe na haswa zikinilenga mimi binafsi. Nafahamu kiu ya wasioitakia mema nchi yetu kuiona POAC ikivunjwa au sura zikibadilishwa kwa kuwa kamati hii imekuwa mwiba kwa mikakati yao ya kifisadi.”
“Kwa maoni yangu, POAC isihusishwe na tuhuma hizi kwa vyovyote vile. Niko tayari nihukumiwe mimi (Zitto) na siyo kuhusisha wajumbe wengine ambao hawatajwi mahala popote katika tuhuma hizi mbaya sana katika historia ya Bunge letu.”
“Nitakuwa tayari kunusuru Kamati ya POAC na masilahi ya taifa letu kwa kujiuzulu uenyekiti, iwapo itathibitika pasipo shaka kuwa nimehongwa. Kamati ya POAC ni muhimu kuliko mimi.”
Awali, Zitto alisema amelazimika kuzungumzia suala hilo kuufahamisha umma kwamba tuhuma hizo zenye shinikizo la kisiasa zinaelekezwa kwake binafsi na si kamati kwa jumla wake.
“Taarifa hizo, kama kawaida ya uzushi mwingine wowote, zimesambazwa kimkakati na kwa kasi kubwa, kiasi cha kuukanganya umma,” alisema.
Alisema mkakati wa kumuunganisha na baadhi ya wabunge wanaotuhumiwa kupokea rushwa, unatekelezwa kwa njia mbalimbali, ikiwamo kauli za watendaji wa Serikali aliodai wamekuwa wakizieneza kutoa taswira kwamba baadhi hoja zake zinatokana na ushawishi wa rushwa.
Akifafanua tuhuma za ushiriki wake wa rushwa katika sekta ya Nishati na Madini, Zitto alisema baada ya Bodi ya Wakurugenzi ya Tanesco kumsimamisha Mkurugenzi Mkuu, William Mhando, POAC ilimwomba Spika aridhie kamati yake iwaite wajumbe wa bodi hiyo ya Tanesco, CAG na PPRA, kujiridhisha na tuhuma hizo.
“POAC ilimwomba Spika kuwaita wahusika kwa kuwa zilikuwapo tetesi kuwa kusimamishwa kazi kwa mkurugenzi huyo kabla ya Bajeti ya Nishati na Madini kulikuwa na lengo la kufunika ‘madudu’ makubwa zaidi, kwa kulichagiza Bunge na tukio hilo dogo, mkakati ambao naona umefanikiwa sana,” alisema na kuongeza:
“Isitoshe, kamati kujiridhisha na hatua za bodi ni sehemu ya msingi ya utekelezaji wa majukumu yake yaliyowekwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge pia Tanesco ni moja ya mashirika ambayo yanawajibika kwetu kwa hesabu zake na ufanisi wake kwa jumla. Tumefanya hivyo katika mashirika mengi na hili la Tanesco siyo tukio la kipekee.”
“Binafsi sijawahi kuwa na mawasiliano ya aina yeyote na uongozi wa Tanesco, kushawishiwa juu ya hatua ambazo POAC ndiyo imezichukua za kutaka kujiridhisha juu ya utaratibu waliotumia.”
“Ieleweke wazi kabisa kuwa hakuna wakati wowote, popote ambapo mimi au kamati yetu imekataa Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco kuchunguzwa kwa tuhuma zozote. Ambacho tumesisitiza wakati wote ni ufuatwaji wa taratibu, kanuni na sheria, hili nitalisimamia iwe masika au kiangazi.”
Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema alisema kutokana na imani hiyo, anaunga mkono suala la tuhuma za rushwa zinazotajwa zichunguzwe na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kina.
“Nakiomba pia chama changu, Chadema na vyombo vya dola vichunguze tuhuma hizo na kujiridhisha na ninaahidi kushiriki kikamilifu, iwapo nitatakiwa katika uchunguzi wowote utakaofanywa na niko tayari kuwajibika iwapo nitakutwa na hatia yoyote,” alisema.
“Napenda kuwatoa hofu wananchi wa Jimbo la Kigoma Kaskazini walionituma kuja kuwawakilisha hapa bungeni na Watanzania wote kwa jumla kwamba, mimi Zitto Kabwe sina bei, sijawahi kuwa nayo na sitarajii kuwa nayo huko mbeleni.”
“Daima nasimamia kidete maadili ya uongozi bora katika maisha yangu yote ya siasa na ninaahidi, sitarudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa katika nchi hii pamoja na mikakati ya aina hii ya kunidhoofisha na kunivunja moyo.”
Zitto alilaani kile alichosema kuwa tabia iliyoanza kujengeka katika siku za hivi karibuni ya kuwamaliza wanasiasa wenye kudai uwajibikaji na uzalendo na kuanzishwa kiwanda kwenye medani ya siasa cha kuzalisha majungu na fitina, zenye lengo la kuwachonganisha wanasiasa wa aina hiyo na wananchi kwa kutumia nguvu za fedha.
Awashukia Profesa Muhongo, Maswi
Aliongeza kwamba, akiwa Dodoma amewahi kupata taarifa kwamba Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wake, Eliachim Maswi ndiyo wanaosambaza taarifa kwamba amepewa rushwa na Tanesco.
“Hali hii inaniondolea shaka juu ya ushiriki wao katika kueneza au kuthibitisha uvumi huo. “Ninajaribu sana kuzuia kutokuwa na shaka na ushiriki wao huo ikizingatiwa uzito na taswira ya nafasi zao katika jamii, lakini wameshindwa kunidhihirishia tofauti,” alisema.
Mbali na kuwatuhumu watendaji hao wa Serikali kwa kumchafua, Zitto alieleza kushangazwa na kauli zao kwamba mgawo wa umeme sasa basi, akieleza kuwa si kweli.
“Ili kumaliza tatizo la mgawo wa umeme kama alivyosema waziri na katibu mkuu, tunapaswa kuwa na Sh42 bilioni kila mwezi kuzilipa kampuni za IPTL na Symbion kama ‘service charge’, fedha hiyo haijatengwa kwenye Bajeti. Sasa msishangae baada ya wiki mbili mgawo ukarejea na watu watasema hizo ni njama za mafisadi,” alisema.
Zitto alisema waziri pia hakuwa sahihi kueleza kuwa Tanesco inapoteza Sh40 bilioni zinazotokana na mapato yake kwa mwezi baada ya matumizi ya Sh11 bilioni kwa kuwa hadi sasa shirika hilo la umma lina madeni mengi.
“Hivi inawezekana kweli maelezo hayo ya waziri kwamba kila mwezi Tanesco inatumia Sh11 bilioni kulipa mishahara na kupoteza Sh40 bilioni, zinazotokana na mapato yake? CAG yuko wapi na Kamati hii (POAC) iko wapi? Yaani wote sisi tusiyaone hayo ila yeye?,” alihoji.
Akizungumzia madai hayo ya Zitto, Profesa Sospeter Muhongo alisema: “Kila wakati tumekuwa tukizungumza juu ya jambo hilo, lakini hata hivyo, kama mnaweza kuangalia kupima uzito uko pande gani basi andikeni upande huo kati ya mimi na Zitto.”
Alisisitiza kwamba hakuna mgawo wa umeme na hilo ndilo analotaka Watanzania wafahamu na waondoe shaka na kamwe wasitegemee kusikiliza mawazo kutoka kwa watu ambao wanaamini kwa kufanya hivyo watajenga umaarufu.
Maswi hakupatikana jana kuzungumzia tuhuma hizo za Zitto baada ya simu yake ya mkononi kuita muda mwingi bila kupokewa na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi hakujibu.
Kwa sababu hiyo, amepinga maoni ya baadhi ya wabunge wanaotaka ivunjwe na badala yake akasema kama kuna ushahidi wa kutosha dhidi ya vitendo vya rushwa, basi awajibike yeye.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Zitto alisema licha ya mkakati huo, katu hatarudi nyuma katika kutetea masilahi ya taifa kwa kuwa anaamini siku zote uongo hujitenga na ukweli.
“Mchango wa POAC katika Bunge na ustawi wa mashirika ya umma ni bayana na haujawahi kutiliwa shaka. Kamati yetu imeokoa upotevu mkubwa wa mali na fedha za umma kutokana na umakini wake,” alisema Zitto na kuongeza:
“Tumefanya hivyo CHC, Kiwira na kwenye mashirika mengi. Kote huku uadilifu wa kamati hii haujawahi kuhojiwa. Zipo hoja pandikizi za kutaka POAC ivunjwe na haswa zikinilenga mimi binafsi. Nafahamu kiu ya wasioitakia mema nchi yetu kuiona POAC ikivunjwa au sura zikibadilishwa kwa kuwa kamati hii imekuwa mwiba kwa mikakati yao ya kifisadi.”
“Kwa maoni yangu, POAC isihusishwe na tuhuma hizi kwa vyovyote vile. Niko tayari nihukumiwe mimi (Zitto) na siyo kuhusisha wajumbe wengine ambao hawatajwi mahala popote katika tuhuma hizi mbaya sana katika historia ya Bunge letu.”
“Nitakuwa tayari kunusuru Kamati ya POAC na masilahi ya taifa letu kwa kujiuzulu uenyekiti, iwapo itathibitika pasipo shaka kuwa nimehongwa. Kamati ya POAC ni muhimu kuliko mimi.”
Awali, Zitto alisema amelazimika kuzungumzia suala hilo kuufahamisha umma kwamba tuhuma hizo zenye shinikizo la kisiasa zinaelekezwa kwake binafsi na si kamati kwa jumla wake.
“Taarifa hizo, kama kawaida ya uzushi mwingine wowote, zimesambazwa kimkakati na kwa kasi kubwa, kiasi cha kuukanganya umma,” alisema.
Alisema mkakati wa kumuunganisha na baadhi ya wabunge wanaotuhumiwa kupokea rushwa, unatekelezwa kwa njia mbalimbali, ikiwamo kauli za watendaji wa Serikali aliodai wamekuwa wakizieneza kutoa taswira kwamba baadhi hoja zake zinatokana na ushawishi wa rushwa.
Akifafanua tuhuma za ushiriki wake wa rushwa katika sekta ya Nishati na Madini, Zitto alisema baada ya Bodi ya Wakurugenzi ya Tanesco kumsimamisha Mkurugenzi Mkuu, William Mhando, POAC ilimwomba Spika aridhie kamati yake iwaite wajumbe wa bodi hiyo ya Tanesco, CAG na PPRA, kujiridhisha na tuhuma hizo.
“POAC ilimwomba Spika kuwaita wahusika kwa kuwa zilikuwapo tetesi kuwa kusimamishwa kazi kwa mkurugenzi huyo kabla ya Bajeti ya Nishati na Madini kulikuwa na lengo la kufunika ‘madudu’ makubwa zaidi, kwa kulichagiza Bunge na tukio hilo dogo, mkakati ambao naona umefanikiwa sana,” alisema na kuongeza:
“Isitoshe, kamati kujiridhisha na hatua za bodi ni sehemu ya msingi ya utekelezaji wa majukumu yake yaliyowekwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge pia Tanesco ni moja ya mashirika ambayo yanawajibika kwetu kwa hesabu zake na ufanisi wake kwa jumla. Tumefanya hivyo katika mashirika mengi na hili la Tanesco siyo tukio la kipekee.”
“Binafsi sijawahi kuwa na mawasiliano ya aina yeyote na uongozi wa Tanesco, kushawishiwa juu ya hatua ambazo POAC ndiyo imezichukua za kutaka kujiridhisha juu ya utaratibu waliotumia.”
“Ieleweke wazi kabisa kuwa hakuna wakati wowote, popote ambapo mimi au kamati yetu imekataa Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco kuchunguzwa kwa tuhuma zozote. Ambacho tumesisitiza wakati wote ni ufuatwaji wa taratibu, kanuni na sheria, hili nitalisimamia iwe masika au kiangazi.”
Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kwa tiketi ya Chadema alisema kutokana na imani hiyo, anaunga mkono suala la tuhuma za rushwa zinazotajwa zichunguzwe na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kina.
“Nakiomba pia chama changu, Chadema na vyombo vya dola vichunguze tuhuma hizo na kujiridhisha na ninaahidi kushiriki kikamilifu, iwapo nitatakiwa katika uchunguzi wowote utakaofanywa na niko tayari kuwajibika iwapo nitakutwa na hatia yoyote,” alisema.
“Napenda kuwatoa hofu wananchi wa Jimbo la Kigoma Kaskazini walionituma kuja kuwawakilisha hapa bungeni na Watanzania wote kwa jumla kwamba, mimi Zitto Kabwe sina bei, sijawahi kuwa nayo na sitarajii kuwa nayo huko mbeleni.”
“Daima nasimamia kidete maadili ya uongozi bora katika maisha yangu yote ya siasa na ninaahidi, sitarudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa katika nchi hii pamoja na mikakati ya aina hii ya kunidhoofisha na kunivunja moyo.”
Zitto alilaani kile alichosema kuwa tabia iliyoanza kujengeka katika siku za hivi karibuni ya kuwamaliza wanasiasa wenye kudai uwajibikaji na uzalendo na kuanzishwa kiwanda kwenye medani ya siasa cha kuzalisha majungu na fitina, zenye lengo la kuwachonganisha wanasiasa wa aina hiyo na wananchi kwa kutumia nguvu za fedha.
Awashukia Profesa Muhongo, Maswi
Aliongeza kwamba, akiwa Dodoma amewahi kupata taarifa kwamba Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wake, Eliachim Maswi ndiyo wanaosambaza taarifa kwamba amepewa rushwa na Tanesco.
“Hali hii inaniondolea shaka juu ya ushiriki wao katika kueneza au kuthibitisha uvumi huo. “Ninajaribu sana kuzuia kutokuwa na shaka na ushiriki wao huo ikizingatiwa uzito na taswira ya nafasi zao katika jamii, lakini wameshindwa kunidhihirishia tofauti,” alisema.
Mbali na kuwatuhumu watendaji hao wa Serikali kwa kumchafua, Zitto alieleza kushangazwa na kauli zao kwamba mgawo wa umeme sasa basi, akieleza kuwa si kweli.
“Ili kumaliza tatizo la mgawo wa umeme kama alivyosema waziri na katibu mkuu, tunapaswa kuwa na Sh42 bilioni kila mwezi kuzilipa kampuni za IPTL na Symbion kama ‘service charge’, fedha hiyo haijatengwa kwenye Bajeti. Sasa msishangae baada ya wiki mbili mgawo ukarejea na watu watasema hizo ni njama za mafisadi,” alisema.
Zitto alisema waziri pia hakuwa sahihi kueleza kuwa Tanesco inapoteza Sh40 bilioni zinazotokana na mapato yake kwa mwezi baada ya matumizi ya Sh11 bilioni kwa kuwa hadi sasa shirika hilo la umma lina madeni mengi.
“Hivi inawezekana kweli maelezo hayo ya waziri kwamba kila mwezi Tanesco inatumia Sh11 bilioni kulipa mishahara na kupoteza Sh40 bilioni, zinazotokana na mapato yake? CAG yuko wapi na Kamati hii (POAC) iko wapi? Yaani wote sisi tusiyaone hayo ila yeye?,” alihoji.
Akizungumzia madai hayo ya Zitto, Profesa Sospeter Muhongo alisema: “Kila wakati tumekuwa tukizungumza juu ya jambo hilo, lakini hata hivyo, kama mnaweza kuangalia kupima uzito uko pande gani basi andikeni upande huo kati ya mimi na Zitto.”
Alisisitiza kwamba hakuna mgawo wa umeme na hilo ndilo analotaka Watanzania wafahamu na waondoe shaka na kamwe wasitegemee kusikiliza mawazo kutoka kwa watu ambao wanaamini kwa kufanya hivyo watajenga umaarufu.
Maswi hakupatikana jana kuzungumzia tuhuma hizo za Zitto baada ya simu yake ya mkononi kuita muda mwingi bila kupokewa na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi hakujibu.
Spika aunda kamati maalum kuchunguza ufisadi bungeni...
KAMATI YA MAADILI YAWEKWA KANDO,KUKAMILISHA KAZI KWA WIKI MBILI...
SAKATA la tuhuma za ufisadi bungeni limeingia katika hatua mpya, baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuamua kuunda Kamati ndogo ya watu watano kuchunguza tuhuma za baadhi ya wabunge kuhongwa, kwa lengo la kushawishi uamuzi unaofaa kuchukulia katika chombo hicho cha kutunga sheria.
Uamuzi huo ambao Spika aliutangaza jana baada ya kipindi cha maswali na majibu Bungeni, unauweka kando ule wa awali, ambao ulikuwa ni kulipeleka suala hilo katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, ambapo alikuwa ameahidi kuwaengua wote watakaoonekana kuwa, wana mgongano wa kimaslahi na suala linalotakiwa kuchunguzwa.
Habari ambazo gazeti hili lilizipata zinadai kuwa, hadi jana wakati Makinda akichukua uamuzi huo, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ilikuwa imeishaanza kazi kwa kufanya vikao kadhaa vya kuainisha watu ambao walipaswa kuitwa ili kutoa ushahidi na wengine kwa ajili ya kujibu tuhuma dhidi yao.
Makinda alisema Kamati hiyo itakayoongozwa na Mbunge wa Mlalo, Brigedia Jenerali Hassan Ngwilizi, itachunguza ukweli wa tuhuma hizo na kutoa majibu kwake ndani ya siku 14 kuanzia jana.
Alisema ameamua kufanya mabadiliko ya namna ya kushughulikia tuhuma hizo ili kutenda haki kutokana na unyeti wa suala hilo.
"Kwa kuzingatia misingi ya haki asili, tumeamua kutomweka mjumbe yeyote wa Kamati ya Nishati na Madini katika kamati hiyo," alisema Spika Makinda na kuongeza;
"Wajumbe wa kamati hiyo ni Mheshimiwa John Chiligati (Manyoni Magharibi), Riziki Omar Juma (Viti maalum), Said Amour Arfi (Mpanda Mjini) na Gosbert Blandes (Karagwe)."
Hata hivyo wajumbe wanne kati ya watano wanatoka ndani ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, isipokuwa Chiligati ambaye anaungana na wenzake akitokea katika Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
Spika alibainisha kuwa, kamati hiyo imepewa majukumu ya kuchunguza tuhuma hizo na kujiridhisha kuhusu ukweli wake, kisha kumshauri (Spika) hatua za kuchukua.
Hatua hiyo ya Spika imekuja siku chache baada ya baadhi ya vyama vya siasa na wabunge, kuhoji usafi wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge hata ikapewa jukumu la kuchunguza tuhuma hizo.
Baadhi ya vyama vilivyoitilia shaka kamati hiyo ni NCCR Mageuzi, ambacho Mwenyekiti wake, James Mbatia alitaka Kamati hiyo pia ivunjwe na kuchunguzwa kwa tuhuma za ufisadi.
Chama kingine ni Chadema, ambapo mwanachama na Mnadhimu Mkuu wa kambi ya upinzani, Tundu Lissu alitaka zivunjwe kamati kadhaa badala ya kamati ya Nishati na Madini pekee.
Pia Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari aliomba mwongozo wa Spika akitaka Kamati za Bunge za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na ile ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), zivunjwe kwani tayari zilishatuhumiwa kwa rushwa.
Hadidu rejea
Spika Makinda alisema kuwa, moja ya majukumu ya msingi ya kamati ya kina Ngwilizi ni kukutana na kukubaliana namna ya kuendesha uchunguzi huo kwa haki na weledi.
"Kamati hiyo itatakiwa kupitia kumbukumbu ya taarifa rasmi za Bunge (Hansard) ili kujua michango ya wabunge wakati wa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, kuwaita na kuwahoji mashahidi," alisema Spika Makinda.
Spika Makinda alimtaja Tundu Lissu kuwa ni shahidi muhimu katika uchunguzi huo, kutokana na hatua yake ya kuwataja baadhi ya watuhumiwa katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma.
Aliwataja mashahidi wengine katika uchunguzi huo kuwa ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, wabunge wote waliochangia Hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini na kutoa tuhuma za rushwa na mbunge yeyote mwenye ushahidi.
"Tundu Lissu ni shahidi kwa sababu aliwahi kuwataja wabunge hao kwenye mkutano wake na waandishi wa habari na waziri ndiye aliyeanzisha tuhuma hizo bungeni," Spika Makinda alisema.
Aliongeza kuwa, kutokana na unyeti wa suala hilo, kamati hiyo inapaswa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni za Bunge na weledi wa hali ya juu.
"Sasa waliotaka kuwataja wabunge hao humo bungeni sasa waende wakawataje kwenye kamati hiyo, alisema Spika Makinda," alisema.
Hata hivyo, jana mchana wakati wa kuahirishwa kikao cha Bunge cha mchana mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali alihoji sababu za kamati hiyo kujaa wabunge watatu wa CCM huku chama chake kikiwa hakina hata mjumbe mmoja.
Lakini, hoja hiyo ilifafanua na mwenyekiti Jenister Mhagama aliyekuwa akiendesha Bunge kwani alisema isingekuwa rahisi kamati hiyo kujaza watu wengi.
SAKATA la tuhuma za ufisadi bungeni limeingia katika hatua mpya, baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuamua kuunda Kamati ndogo ya watu watano kuchunguza tuhuma za baadhi ya wabunge kuhongwa, kwa lengo la kushawishi uamuzi unaofaa kuchukulia katika chombo hicho cha kutunga sheria.
Uamuzi huo ambao Spika aliutangaza jana baada ya kipindi cha maswali na majibu Bungeni, unauweka kando ule wa awali, ambao ulikuwa ni kulipeleka suala hilo katika Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, ambapo alikuwa ameahidi kuwaengua wote watakaoonekana kuwa, wana mgongano wa kimaslahi na suala linalotakiwa kuchunguzwa.
Habari ambazo gazeti hili lilizipata zinadai kuwa, hadi jana wakati Makinda akichukua uamuzi huo, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ilikuwa imeishaanza kazi kwa kufanya vikao kadhaa vya kuainisha watu ambao walipaswa kuitwa ili kutoa ushahidi na wengine kwa ajili ya kujibu tuhuma dhidi yao.
Makinda alisema Kamati hiyo itakayoongozwa na Mbunge wa Mlalo, Brigedia Jenerali Hassan Ngwilizi, itachunguza ukweli wa tuhuma hizo na kutoa majibu kwake ndani ya siku 14 kuanzia jana.
Alisema ameamua kufanya mabadiliko ya namna ya kushughulikia tuhuma hizo ili kutenda haki kutokana na unyeti wa suala hilo.
"Kwa kuzingatia misingi ya haki asili, tumeamua kutomweka mjumbe yeyote wa Kamati ya Nishati na Madini katika kamati hiyo," alisema Spika Makinda na kuongeza;
"Wajumbe wa kamati hiyo ni Mheshimiwa John Chiligati (Manyoni Magharibi), Riziki Omar Juma (Viti maalum), Said Amour Arfi (Mpanda Mjini) na Gosbert Blandes (Karagwe)."
Hata hivyo wajumbe wanne kati ya watano wanatoka ndani ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, isipokuwa Chiligati ambaye anaungana na wenzake akitokea katika Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
Spika alibainisha kuwa, kamati hiyo imepewa majukumu ya kuchunguza tuhuma hizo na kujiridhisha kuhusu ukweli wake, kisha kumshauri (Spika) hatua za kuchukua.
Hatua hiyo ya Spika imekuja siku chache baada ya baadhi ya vyama vya siasa na wabunge, kuhoji usafi wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge hata ikapewa jukumu la kuchunguza tuhuma hizo.
Baadhi ya vyama vilivyoitilia shaka kamati hiyo ni NCCR Mageuzi, ambacho Mwenyekiti wake, James Mbatia alitaka Kamati hiyo pia ivunjwe na kuchunguzwa kwa tuhuma za ufisadi.
Chama kingine ni Chadema, ambapo mwanachama na Mnadhimu Mkuu wa kambi ya upinzani, Tundu Lissu alitaka zivunjwe kamati kadhaa badala ya kamati ya Nishati na Madini pekee.
Pia Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari aliomba mwongozo wa Spika akitaka Kamati za Bunge za Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na ile ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), zivunjwe kwani tayari zilishatuhumiwa kwa rushwa.
Hadidu rejea
Spika Makinda alisema kuwa, moja ya majukumu ya msingi ya kamati ya kina Ngwilizi ni kukutana na kukubaliana namna ya kuendesha uchunguzi huo kwa haki na weledi.
"Kamati hiyo itatakiwa kupitia kumbukumbu ya taarifa rasmi za Bunge (Hansard) ili kujua michango ya wabunge wakati wa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, kuwaita na kuwahoji mashahidi," alisema Spika Makinda.
Spika Makinda alimtaja Tundu Lissu kuwa ni shahidi muhimu katika uchunguzi huo, kutokana na hatua yake ya kuwataja baadhi ya watuhumiwa katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma.
Aliwataja mashahidi wengine katika uchunguzi huo kuwa ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, wabunge wote waliochangia Hotuba ya Wizara ya Nishati na Madini na kutoa tuhuma za rushwa na mbunge yeyote mwenye ushahidi.
"Tundu Lissu ni shahidi kwa sababu aliwahi kuwataja wabunge hao kwenye mkutano wake na waandishi wa habari na waziri ndiye aliyeanzisha tuhuma hizo bungeni," Spika Makinda alisema.
Aliongeza kuwa, kutokana na unyeti wa suala hilo, kamati hiyo inapaswa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni za Bunge na weledi wa hali ya juu.
"Sasa waliotaka kuwataja wabunge hao humo bungeni sasa waende wakawataje kwenye kamati hiyo, alisema Spika Makinda," alisema.
Hata hivyo, jana mchana wakati wa kuahirishwa kikao cha Bunge cha mchana mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali alihoji sababu za kamati hiyo kujaa wabunge watatu wa CCM huku chama chake kikiwa hakina hata mjumbe mmoja.
Lakini, hoja hiyo ilifafanua na mwenyekiti Jenister Mhagama aliyekuwa akiendesha Bunge kwani alisema isingekuwa rahisi kamati hiyo kujaza watu wengi.
Wanasayansi waazimia kuuangamiza Ukimwi,,,,,,,,,,,,,,
MBINU MPYA ZA KITAALAMU SASA KUTUMIKA DUNIA NZIMA ......................
MKUTANO wa Ukimwi uliokuwa unafanyika Washington DC, Marekani umemalizika kwa wajumbe zaidi ya 2,000 kuridhia maendeleo ya kisayansi yaliyofikiwa kwa sasa wakisema ni madhubuti hivyo kutoa azimio la kuungana kuangamiza janga la maradhi hayo duniani. Moja ya maazimio yao ni kuifikisha dunia mahali ambako hakutakuwa na mtu atakayekufa wala atakayekuwa anaishi na Virusi Vya Ukimwi (VVU). Hii inatokana na matumaini ya kisayansi waliyohakikishiwa na watafiti juu ya kuwepo kwa dawa zinazoweza kuzuia maambukizo mapya na ambazo zikitumika kikamilifu zaweza kufanya kazi kama tiba.
Pamoja na kuwepo kwa dawa hizo, wamekiri kuwa mkakati huo hauwezi kufikiwa iwapo dunia haitajenga mshikamano wa pamoja wa kisera, uelimishaji na fedha za kutosha kufanikisha mbinu hizo mpya za kisayansi. Wanasayansi wametahadharisha kuwa kuwepo kwa dawa hiyo siyo tija ya kuumaliza Ukimwi kama mikakati imara haitawekwa dunia nzima. Rais wa Taasisi ya Kijamii ya Kimataifa ya Mapambano dhidi ya VVU (IAS), Dk Elly Katabira alisema yapo mambo mengi ambayo yalithibitishwa kisayansi huko nyuma lakini kwa kuwa hakukuwa na mikakati madhubuti, tatizo hilo limeendelea kuwa janga la dunia.
Dk Katabira ambaye pia ni mmoja wa watafiti wa kisayansi katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Makerere, Uganda alitoa mfano wa watoto kuendelea kuambukizwa Ukimwi wanapozaliwa wakati tayari dawa ya kuondoa tatizo hilo ipo. “Ni jambo la kusikitisha kwamba dawa ya kuzuia maambukizo ya VVU tumekuwa nayo tangu miaka 1990 lakini mwaka huu, 2012 takwimu zinaonyesha kuwa watoto zaidi ya 300,000 wataambukizwa VVU wakati wa kuzaliwa,” alisema Dk Katabira, ambaye pia alikuwa ni Mwenyekiti wa mkutano huo wa Ukimwi uliomalizika wiki iliyopita.
Kwa sababu hiyo, akasema silaha za kupambana na Ukimwi kwa sasa zipo lakini kama hakuna mikakati madhubuti ya kuzitumia, bado utaendelea kuwa janga la dunia. Mkutano huo wa kimataifa wa Ukimwi umekuwa ukifanyika kila mwaka ukiwakutanisha wanasayansi na watunga sera kama vile wanasiasa na wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa huo uliogundulika kwa mara ya kwanza mwaka 1981.
Mkutano wa safari hii umeelezewa kuwa ni wa kipekee zaidi ukilinganishwa na ile iliyowahi kufanyika miaka 30 iliyopita kwani kwa mara ya kwanza, umethubutu kutamka wazi, “dawa ya kuangamiza kabisa janga la Ukimwi ipo.” Kutokana na kujiamini huko, mkutano huo umetoka na Azimio linaloitwa la Washington DC ambalo ni la kugeuza kauli ya kuwa “Ukimwi hauna dawa” na kuwa “Ni wakati wa kuangamiza janga la Ukimwi.”
Azimio hilo ambalo tayari limetafsiriwa katika lugha mbalimbali duniani, kikiwemo Kiswahili, linasema: “Kugeuza mkono kwa pamoja: Ilani ya kuangamiza janga la Ukimwi.” Linaeleza: “Tuko katika wakati wa kipekee katika historia ya janga la Ukimwi. Miongo mitatu ya upiganiaji, utafiti na utoaji wa huduma stahimilivu kwa jamii imeifikisha dunia katika hali ambayo haikuwazika miaka iliyopita.” “Kwa sasa kuna uwezekano wa kuanza kuangamiza janga la Ukimwi wakati wetu.
Hasara imekuwa ya kutohesabika… Lakini sasa, kupitia maendeleo mapya ya kisayansi… Tumegundua kwamba inawezekana kukusanya mbinu zilizothibitishwa, ambazo, kama zitatekelezwa ipasavyo, zinaweza kugeuza mkondo wa Ukimwi.” Ingawa tafiti za kisayansi zinaendelea na baadhi zikiwa na matumaini mazuri ya kupata dawa ya chanjo na kuponya waathirika dhidi ya VVU, bado hazijathibitishwa na azimio la mkutano huo limeridhia mbinu zilizowasilishwa na wanasayansi za kuzuia maambukizo.
Imeelezwa kwamba mbinu hizo mpya za kuzuia kusambaa kwa VVU zikitumika kikamilifu siyo tu zitazuia maambukizo mapya, bali zitatibu wale waliokwishaambukizwa. Moja ya mikakati ya kufanikisha azimio hilo ni kuhakikisha duniani kote vinapatikana vifaa bora vya kuchunguza VVU na upatikanaji wa dawa. “Lazima tuongeze rasilimali na bidii yetu kwa kutumia vifaa tulivyonavyo leo kuzuia maambukizo mapya na kuboresha afya ya mamilioni ya watu walio na VVU/Ukimwi. Mamilioni ya maisha yataokolewa,” inaeleza sehemu ya Azimio hilo la Washington DC na kuongeza:
“Lengo la kwanza ni kuangamiza janga la Ukimwi... Liko katika uwezo wetu... Hakuna mtu anapaswa kutengwa ikiwa tunapanga kufikia lengo letu.” Miongoni mwa mambo ambayo azimio hilo linasisitiza kuwa hayana budi kuzingatiwa ili kuleta usawa ni pamoja na kuondoa unyanyapaa, ubaguzi, vikwazo vya kisheria na unyanyasaji wa haki za waathirika na wale walio hatarini. “Unyanyapaa na ubaguzi unazuia juhudi zetu zote na kuzuia utoaji wa huduma muhimu. Tuongeze kwa dhahiri upimwaji wa VVU, utoaji ushauri na uhusiano wa kinga, huduma za kuponya na usaidizi. Kila mtu ana haki ya kujua hali yake ya VVU na kupata matibabu, dawa na usaidizi,” linasisitiza azimio hilo.
Malengo mengine ni kutoa matibabu kwa wanawake wote wajawazito na wanaonyonyesha wanaoishi na VVU na kuangamiza uambukizaji wakati wa kujifungua. Azimio linahamasisha ujengaji wa mtandao mpana wa vita hiyo kwa kusema: “Tuongeze ufikio wa matibabu ya kupunguza makali ya VVU/Ukimwi kwa wote wanaohitaji.
Hatuwezi kuangamiza Ukimwi mpaka mikakati hii iweze kutekelezeka ulimwenguni kote.” Linaongeza: “ Tuharakishe utafiti kuhusu vifaa vipya vya kukinga na kutibu VVU, ikiwa ni pamoja na njia mpya kama vile tiba ya kuzuia maradhi kabla ya kuambukizwa (PrEP) na vizuizi vya vijiumbe maradhi na utoaji bora wa kile tunachojua kinafanya kazi ipasavyo; kuanzia kondomu mpaka matibabu kama kinga.
Tuongeze utafiti wa dawa ya chanjo na dawa ya kuponya. Utafiti ni muhimu kwa kutusaidia kupigana na janga hili.” Tayari Dawa ya Kupunguza Makali ya VVU (ARV) ya Truvada iliyonza kutumika duniani tangu 2004, wiki chache zilizopita ilithibitishwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa Marekani (FDA), kuwa ina uwezo wa kuzuia mtu aliyeathirika kumwambukiza mwenzi wake atakayeshiriki naye tendo la ndoa bila kutumia kondomu. Zipo aina kadhaa ya dawa za chanjo na tiba zilizowasilishwa kwenye mkutano huo pamoja na ushahidi wa jinsi zinavyoponya lakini bado hazijathibitishwa kutumika kimataifa.
MKUTANO wa Ukimwi uliokuwa unafanyika Washington DC, Marekani umemalizika kwa wajumbe zaidi ya 2,000 kuridhia maendeleo ya kisayansi yaliyofikiwa kwa sasa wakisema ni madhubuti hivyo kutoa azimio la kuungana kuangamiza janga la maradhi hayo duniani. Moja ya maazimio yao ni kuifikisha dunia mahali ambako hakutakuwa na mtu atakayekufa wala atakayekuwa anaishi na Virusi Vya Ukimwi (VVU). Hii inatokana na matumaini ya kisayansi waliyohakikishiwa na watafiti juu ya kuwepo kwa dawa zinazoweza kuzuia maambukizo mapya na ambazo zikitumika kikamilifu zaweza kufanya kazi kama tiba.
Pamoja na kuwepo kwa dawa hizo, wamekiri kuwa mkakati huo hauwezi kufikiwa iwapo dunia haitajenga mshikamano wa pamoja wa kisera, uelimishaji na fedha za kutosha kufanikisha mbinu hizo mpya za kisayansi. Wanasayansi wametahadharisha kuwa kuwepo kwa dawa hiyo siyo tija ya kuumaliza Ukimwi kama mikakati imara haitawekwa dunia nzima. Rais wa Taasisi ya Kijamii ya Kimataifa ya Mapambano dhidi ya VVU (IAS), Dk Elly Katabira alisema yapo mambo mengi ambayo yalithibitishwa kisayansi huko nyuma lakini kwa kuwa hakukuwa na mikakati madhubuti, tatizo hilo limeendelea kuwa janga la dunia.
Dk Katabira ambaye pia ni mmoja wa watafiti wa kisayansi katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Makerere, Uganda alitoa mfano wa watoto kuendelea kuambukizwa Ukimwi wanapozaliwa wakati tayari dawa ya kuondoa tatizo hilo ipo. “Ni jambo la kusikitisha kwamba dawa ya kuzuia maambukizo ya VVU tumekuwa nayo tangu miaka 1990 lakini mwaka huu, 2012 takwimu zinaonyesha kuwa watoto zaidi ya 300,000 wataambukizwa VVU wakati wa kuzaliwa,” alisema Dk Katabira, ambaye pia alikuwa ni Mwenyekiti wa mkutano huo wa Ukimwi uliomalizika wiki iliyopita.
Kwa sababu hiyo, akasema silaha za kupambana na Ukimwi kwa sasa zipo lakini kama hakuna mikakati madhubuti ya kuzitumia, bado utaendelea kuwa janga la dunia. Mkutano huo wa kimataifa wa Ukimwi umekuwa ukifanyika kila mwaka ukiwakutanisha wanasayansi na watunga sera kama vile wanasiasa na wadau wa mapambano dhidi ya ugonjwa huo uliogundulika kwa mara ya kwanza mwaka 1981.
Mkutano wa safari hii umeelezewa kuwa ni wa kipekee zaidi ukilinganishwa na ile iliyowahi kufanyika miaka 30 iliyopita kwani kwa mara ya kwanza, umethubutu kutamka wazi, “dawa ya kuangamiza kabisa janga la Ukimwi ipo.” Kutokana na kujiamini huko, mkutano huo umetoka na Azimio linaloitwa la Washington DC ambalo ni la kugeuza kauli ya kuwa “Ukimwi hauna dawa” na kuwa “Ni wakati wa kuangamiza janga la Ukimwi.”
Azimio hilo ambalo tayari limetafsiriwa katika lugha mbalimbali duniani, kikiwemo Kiswahili, linasema: “Kugeuza mkono kwa pamoja: Ilani ya kuangamiza janga la Ukimwi.” Linaeleza: “Tuko katika wakati wa kipekee katika historia ya janga la Ukimwi. Miongo mitatu ya upiganiaji, utafiti na utoaji wa huduma stahimilivu kwa jamii imeifikisha dunia katika hali ambayo haikuwazika miaka iliyopita.” “Kwa sasa kuna uwezekano wa kuanza kuangamiza janga la Ukimwi wakati wetu.
Hasara imekuwa ya kutohesabika… Lakini sasa, kupitia maendeleo mapya ya kisayansi… Tumegundua kwamba inawezekana kukusanya mbinu zilizothibitishwa, ambazo, kama zitatekelezwa ipasavyo, zinaweza kugeuza mkondo wa Ukimwi.” Ingawa tafiti za kisayansi zinaendelea na baadhi zikiwa na matumaini mazuri ya kupata dawa ya chanjo na kuponya waathirika dhidi ya VVU, bado hazijathibitishwa na azimio la mkutano huo limeridhia mbinu zilizowasilishwa na wanasayansi za kuzuia maambukizo.
Imeelezwa kwamba mbinu hizo mpya za kuzuia kusambaa kwa VVU zikitumika kikamilifu siyo tu zitazuia maambukizo mapya, bali zitatibu wale waliokwishaambukizwa. Moja ya mikakati ya kufanikisha azimio hilo ni kuhakikisha duniani kote vinapatikana vifaa bora vya kuchunguza VVU na upatikanaji wa dawa. “Lazima tuongeze rasilimali na bidii yetu kwa kutumia vifaa tulivyonavyo leo kuzuia maambukizo mapya na kuboresha afya ya mamilioni ya watu walio na VVU/Ukimwi. Mamilioni ya maisha yataokolewa,” inaeleza sehemu ya Azimio hilo la Washington DC na kuongeza:
“Lengo la kwanza ni kuangamiza janga la Ukimwi... Liko katika uwezo wetu... Hakuna mtu anapaswa kutengwa ikiwa tunapanga kufikia lengo letu.” Miongoni mwa mambo ambayo azimio hilo linasisitiza kuwa hayana budi kuzingatiwa ili kuleta usawa ni pamoja na kuondoa unyanyapaa, ubaguzi, vikwazo vya kisheria na unyanyasaji wa haki za waathirika na wale walio hatarini. “Unyanyapaa na ubaguzi unazuia juhudi zetu zote na kuzuia utoaji wa huduma muhimu. Tuongeze kwa dhahiri upimwaji wa VVU, utoaji ushauri na uhusiano wa kinga, huduma za kuponya na usaidizi. Kila mtu ana haki ya kujua hali yake ya VVU na kupata matibabu, dawa na usaidizi,” linasisitiza azimio hilo.
Malengo mengine ni kutoa matibabu kwa wanawake wote wajawazito na wanaonyonyesha wanaoishi na VVU na kuangamiza uambukizaji wakati wa kujifungua. Azimio linahamasisha ujengaji wa mtandao mpana wa vita hiyo kwa kusema: “Tuongeze ufikio wa matibabu ya kupunguza makali ya VVU/Ukimwi kwa wote wanaohitaji.
Hatuwezi kuangamiza Ukimwi mpaka mikakati hii iweze kutekelezeka ulimwenguni kote.” Linaongeza: “ Tuharakishe utafiti kuhusu vifaa vipya vya kukinga na kutibu VVU, ikiwa ni pamoja na njia mpya kama vile tiba ya kuzuia maradhi kabla ya kuambukizwa (PrEP) na vizuizi vya vijiumbe maradhi na utoaji bora wa kile tunachojua kinafanya kazi ipasavyo; kuanzia kondomu mpaka matibabu kama kinga.
Tuongeze utafiti wa dawa ya chanjo na dawa ya kuponya. Utafiti ni muhimu kwa kutusaidia kupigana na janga hili.” Tayari Dawa ya Kupunguza Makali ya VVU (ARV) ya Truvada iliyonza kutumika duniani tangu 2004, wiki chache zilizopita ilithibitishwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa Marekani (FDA), kuwa ina uwezo wa kuzuia mtu aliyeathirika kumwambukiza mwenzi wake atakayeshiriki naye tendo la ndoa bila kutumia kondomu. Zipo aina kadhaa ya dawa za chanjo na tiba zilizowasilishwa kwenye mkutano huo pamoja na ushahidi wa jinsi zinavyoponya lakini bado hazijathibitishwa kutumika kimataifa.
Thursday, August 2, 2012
CREATIVITY.......!!!
THE WAY TO GET GOOD IDEAS IS TO GET LOTS OF IDEAS AND THROW THE BAD ONES AWAY...says the son of maletho!!!
PEACE... Peace of mind attained not by ignoring problems but by solving them....
PEACE... Peace of mind attained not by ignoring problems but by solving them....
Diaspora Writer"Muimbaji Chameleon kutoka Uganda ni Mwizi sana Hapa Uingereza amesha tapeli watu kishenzi,,,,,
Muimbaji chameleon kutoka Uganda ni mwizi sana .Hapa Uingereza amesha tapeli watu kishenzi staili hio hio na maneja wake. Ni mchezo wake.Akirudi hapa UK anaweza kupigwa mawe.Bangi zina msumbua tuu.Yeye ninani mtu amabe hawezi kumuheshimu mwakilishi wa Rais wetu Uganda -Balozi wetu pale kampala.Nashanga serikali ya Uganda wamemsikiliza na kuifanya hii ishu itake kuharibu uhusiano mkubwa kati ya nchi hizi mbili.Hivyo chameleone mnamjua ? juzi kawa muislam kesho yake karutadi tena .Bangi haziwezi zina mpelekesha. Anafaa kua jela maana ni msani jambazi.Huko kampala na sikia wamesha rushiana risasi na msani Bobby wine. Naomba watanzania wote tumzomeye chameleon na asirudi tanzania tena kwa tabia yake tena . Hon membe tunaomba hili ulifanyie kazi kwamba wageni hawezi kuja na wakatu abuse hata nyumbani kwetu. Bwana Erik nawe usije uka shika pasport ya mtu ni document ya serikali wala sio mtu binafsi
Ahsante
Diaspora writer
Ahsante
Diaspora writer
Sunday, July 29, 2012
WABUNGE MAFISADI WATAJWA.....
SPIKA AVUNJA KAMATI YA NISHATI, WAZIRI AELEZA WALIVYOITAFUNA TANESCO.....
WAKATI wabunge wakitoa tuhuma nzito dhidi ya wenzao wanaodaiwa kujihusisha na ufisadi ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), imebainishwa kuwa wabunge wenye tabia hiyo ni watano, watatu kutoka chama tawala CCM na wawili upinzani.
Habari zilizopatikana jana mjini Dodoma zimeeleza kuwa baadhi ya wabunge hao wanatoka katika Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, huku wengine wakitoka Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, wabunge hao wamedaiwa kuwa wamekuwa wakitumia nafasi zao za ubunge na ujumbe wa kamati kufanya biashara na Tanesco na kutetea mafisadi ndani ya shirika hilo la umma.
Gazeti hili limefanikiwa kupata majina ya wabunge hao, ambayo leo hatutayataja kwa sababu za kitaaluma.
Baadhi ya wabunge waliochangia hoja hiyo bungeni juzi na jana walisema kuwa, wanawafahamu wabunge hao kwa majina, lakini hawapendi kuwataja kwa kuwa siyo wakati mwafaka.
Moto wa kutaka kutajwa kwa majina ya wabunge hao ulikolezwa jana na Mbunge Vita Kawawa wa Namtumbo(CCM) aliyeomba Mwongozo wa Spika, akitaka jambo hili lijadiliwe na Bunge na kupendekeza kuwa, Kamati za Bunge zinazotuhumiwa kwa rushwa zivunjwe.
“Waheshimiwa wabunge wamejadili suala hili kwenye wizara, lakini kwa mujibu wa kifungu cha 55 (3)f mbunge au waziri anaweza kutoa hoja ili jambo fulani lijadiliwe. Sasa naomba kutoa hoja ya kujadili suala hilo," Kawawa alisema.
Aliliomba pia Bunge likubali kuivunja na kuiunda upya Kamati ya Nishati na Madini na kamati nyingine zilizolalamikiwa kwa rushwa. Hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge.
Baada ya hoja hiyo kuungwa mkono Spika wa Bunge, Anne Makinda alisimama na kukubali hoja hiyo ya Kawawa na kutangaza kuivunja Kamati ya Nishati na Madini.
Spika Makinda alisema ameiagiza Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge kutengeneza kanuni za kuwadhibiti wabunge wenye tabia hiyo ya kupokea rushwa kutoka kwa watu mbalimbali ili kutimiza matakwa yao binafsi.
"Ninakubali kuivunja Kamati ya Nishati na Madini na zingine ambazo zitatajwa kwenye tuhuma hizo. Nalipeleka pia suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, halafu kama ni kutajwa (wabunge hao), basi tutapata mwongozo wa kamati hiyo." alisema Spika Makinda na kuongeza:
"Nasema kwa dhati kabisa, kitendo hiki hakikubaliki ndani ya Bunge hili. Wabunge mkae vizuri. Kama kuna baadhi yetu wanaenda huku na huku kujitafutia masilahi binafsi, tutawezaje kuisimamia Serikali?"
Mbunge Zedi
Baada ya Spika kutangaza kuvunja Kamati ya Nishati na Madini, Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Seleman Zedi alisema kuwa ameshtushwa na uamuzi huo na anasubiri uamuzi wa Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge.
"Nimeshtushwa sana na uamuzi huo, lakini tusubiri Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge," alisema Zedi.
Waziri Muhongo
Akihitimisha hoja ya wizara yake bungeni jana, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kuwa baadhi ya wabunge ambao wanashiriki kwenye vikao vya uamuzi vya Tanesco kama wajumbe, wamekuwa wakilihujumu shirika hilo kwa njia mbalimbali ikiwamo kufanya nalo biashara.
"Shirika liliwahi kulipa Pauni za Uingereza 50,000 kwa ajili ya kununua vipuri, lakini kilicholetwa nchini ni masanduku ya misumari,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza;
“Hata katika nguzo za umeme kuna biashara inaendelea. Tunajua kuwa nguzo hizo zinazalishwa Iringa na kupelekwa Mombasa kisha kurudishwa nchini kwa maelezo kwamba zimetoka Afrika Kusini."
Waziri Muhongo alisema kuwa mbali na ufisadi huo, baadhi ya wabunge ambao ni wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini wamewahi kuliuzia shirika hilo matairi ya magari kwa bei kubwa, bidhaa ambayo hata hivyo alisema haina ubora unaokubalika.
"Baadhi ya wabunge wanafanya biashara na Tanesco; niseme tu kuwa, hii siyo sahihi. Lakini niombe kwamba mjadala huu tuufunge kwa sababu, tayari tumekabidhi suala hilo kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)" alisema Waziri Muhongo.
Waziri Muhongo pia alizungumzia jinsi baadhi ya watu na kampuni zinavyoiibia Tanesco kupitia mita za Luku ambapo aliwataja watu hao kuwa ni pamoja na Shule za St. Mary's zinazodaiwa Sh10.5 milioni, Access Bank, Tawi la Tabata Matumbi Sh13.8 milioni na Hoteli ya Akudo Paradaise ya Kariakoo inayodaiwa Sh25.5 milioni.
Alisema kuwa baada ya kubainika kwa wadaiwa hao hutumia umeme kinyume na utaratibu,wahusika wote walikamatwa na kufikishwa kituo cha polisi baada ya kufanyika kwa uchunguzi.
“Baada ya kufanya uchunguzi na kubaini kuwapo kwa watu wanaotumia umeme bila kulipia na kuisababishia Tanesco hasara, tumeamua kuwachukulia hatua ikiwamo kuwafikisha polisi,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza:
“Inaonyesha wazi kwamba wizi wa umeme wa Luku umekuwa ukifanyika mara kwa mara na kwamba baada ya kuwakamata hawa, uchunguzi utaendelea na wengine watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.”
Jenista Mhagama
Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama alisema kuwa, amepokea kwa masikitiko taarifa hizo za wabunge wa CCM kuingia katika tuhuma hizo, lakini akasema namna nzuri ya kushughulikia tatizo hilo ni vyombo vya dola kufanya uchunguzi makini ili kujiridhisha na kisha hatua za kisheria kufuatwa.
"Ni taarifa mbaya kwa kweli, lakini mimi niiombe Serikali itusaidie kufanya uchunguzi ili ukweli ubainike na hatua zichukuliwe," alisema Mhagama.
Mbunge Silinde
Naye Katibu wa Wabunge wa Chadema, David Silinde alisema: "Kwa kuwa tumesikia, kama kambi tutafanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo. Tutakaa kikao cha kuamua nini cha kufanya. Pia tutatoa tamko juu ya mwenendo mzima wa hizi tuhuma na Bunge kwa ujumla.”
Zitto
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma ambayo imeunganishwa kwenye tuhuma hizo, Zitto Kabwe, alisema tuhuma hizo anazisikia, lakini anaziona kama siasa za majitaka kwa sababu zinarushwa bila ushahidi wowote.
"Hakuna hata mbunge mmoja aliyesimama kusema nani amehongwa nini. Mimi binafsi sijahongwa na mtu yeyote wala mimi sijamtetea mtu isipokuwa natetea taratibu kufuatwa," alisema.
Zitto alibainisha kuwa anaamini tuhuma hizo zimetokana na hasira za yeye kupinga posho za wabunge na sasa wameona hilo ndilo eneo la kumkomoa.
"Kwa kuwa ‘my conscious is clear’, (dhamira yangu safi) sina mashaka, uzushi, uongo na siasa za majitaka hizi zitaumbuliwa na ukweli. Hata hivyo, kwa kuwa tuhuma hizo zinasemwa juu juu tu, tutataka vyombo vya dola vichunguze na ikithibitika hatua zichukuliwe," alisema na kuongeza:
"Kwangu mimi naona hizi ni siasa za urais na hasira za posho. Wenye kutaka urais wa vyama vyote na wapambe wao, wameungana kunichafulia heshima yangu. Wabunge wenye njaa ya posho, wameungana kunikomoa. Ukweli una tabia ya kutopenda kupuuzwa. Mwalimu Nyerere (Julius) alisema katika andiko lake la 'Tujisahihishe'.”
Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini(Chadema) alishauri pia Spika wa Bunge kutumia Kamati ya Maadili kuchunguza tuhuma hizo kwa kuwa hazipaswi kuachwa zikapita hivihivi.
John Cheyo
Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali, John Cheyo alisema anasikitika kuona Bunge ambalo kimsingi ni kitovu cha uadilifu limeanza kuvamiwa na mafisadi.
"Very unfortunate, (bahati mbaya sana) Bunge ambalo ni kilele cha uadilifu, nyumba ya waheshimiwa, ambako kunatarajiwa high level of intergrity (uadilifu wa hali ya juu), kuanza kutumika kama perpets (vibaraka) wa mafisadi," alisema.
Cheyo aliongeza: "Ninalaani sana kitendo hicho, lakini niwaambie viongozi wapya wa Wizara ya Nishati na Madini kuwa, waendelee kufanya kazi kwa uadilifu na nguvu yao ni wabunge wengi wema, ambao watawaunga mkono. Wasikate tama," alisema.
Mjadala ya wabunge
Mbunge wa Maswa Magharibi (Chadema), John Shibuda aliliomba Bunge kufanya uchunguzi ili kuwabaini wabunge wanaojihusisha na vitendo vya rushwa.
Alisema baadhi ya wabunge wanatumia nafasi zao vibaya kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa ili kuiyumbisha Serikali.
“Namwomba Spika na timu yake yote ikaona kuna haja ya kufanya uchunguzi kwa wabunge ili kuweza kuwabaini wanaotumia nafasi zao vibaya kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa ilikuiyumbisha Serikali ,” alisema Shibuda
Mbuge Kangi
Naye Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora alitaka Waziri wa Nishati na Madini awataje wabunge aliowatuhumu ili kuonyesha usawa hasa baada ya kuwataja kwa majina watuhumiwa wengine katika ufisadi wa Tanesco na wale wanaoliibia umeme shirika hilo la umma.
"Tunaomba waziri asema kwa nini asiwataje hao wengine wakati tayari ametutajia kina Freddy na Veronica William Mhando na taasisi za St Mary? " alihoji.
Hoja hiyo ya Lugora ilitupwa na Spika wa Bunge Anne Makinda aliyesema kuwa jambo hilo lina taratibu zake.
Kamata
Vicky Kimata (Viti Maalumu) nusura amwage machozi bungeni juzi jioni, alipozungumza kwa uchungu kupinga hatua ya wabunge hao kujihusisha na ufisadi, huku akieleza kuwa nchi imefika pabaya.
'Watanzania tumefikia hapo! Watu wanatengeneza mgawo wa umeme ili kujipatia hela, Jamani...jamani.. Hammwogopi hata Mungu!"
Said Mussa Zuberi alipendekeza itungwe sheria ya kuwanyonga mafisadi na wahujumu uchumi kwa kuwa matendo hayo pia ni uuaji.
"Katika taifa letu tuna wadudu sijui tuwaite mchwa ambao wanaharibu yaliyotengenezwa kwa maslahi yao. Nawashauri wananchi kwa kuwa sasa tuko kwenye suala la Katiba, wasisahau kupitisha sheria ili watu wahujumu uchumi tuwaue, tena kwa risasi.
WAKATI wabunge wakitoa tuhuma nzito dhidi ya wenzao wanaodaiwa kujihusisha na ufisadi ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), imebainishwa kuwa wabunge wenye tabia hiyo ni watano, watatu kutoka chama tawala CCM na wawili upinzani.
Habari zilizopatikana jana mjini Dodoma zimeeleza kuwa baadhi ya wabunge hao wanatoka katika Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, huku wengine wakitoka Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, wabunge hao wamedaiwa kuwa wamekuwa wakitumia nafasi zao za ubunge na ujumbe wa kamati kufanya biashara na Tanesco na kutetea mafisadi ndani ya shirika hilo la umma.
Gazeti hili limefanikiwa kupata majina ya wabunge hao, ambayo leo hatutayataja kwa sababu za kitaaluma.
Baadhi ya wabunge waliochangia hoja hiyo bungeni juzi na jana walisema kuwa, wanawafahamu wabunge hao kwa majina, lakini hawapendi kuwataja kwa kuwa siyo wakati mwafaka.
Moto wa kutaka kutajwa kwa majina ya wabunge hao ulikolezwa jana na Mbunge Vita Kawawa wa Namtumbo(CCM) aliyeomba Mwongozo wa Spika, akitaka jambo hili lijadiliwe na Bunge na kupendekeza kuwa, Kamati za Bunge zinazotuhumiwa kwa rushwa zivunjwe.
“Waheshimiwa wabunge wamejadili suala hili kwenye wizara, lakini kwa mujibu wa kifungu cha 55 (3)f mbunge au waziri anaweza kutoa hoja ili jambo fulani lijadiliwe. Sasa naomba kutoa hoja ya kujadili suala hilo," Kawawa alisema.
Aliliomba pia Bunge likubali kuivunja na kuiunda upya Kamati ya Nishati na Madini na kamati nyingine zilizolalamikiwa kwa rushwa. Hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge.
Baada ya hoja hiyo kuungwa mkono Spika wa Bunge, Anne Makinda alisimama na kukubali hoja hiyo ya Kawawa na kutangaza kuivunja Kamati ya Nishati na Madini.
Spika Makinda alisema ameiagiza Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge kutengeneza kanuni za kuwadhibiti wabunge wenye tabia hiyo ya kupokea rushwa kutoka kwa watu mbalimbali ili kutimiza matakwa yao binafsi.
"Ninakubali kuivunja Kamati ya Nishati na Madini na zingine ambazo zitatajwa kwenye tuhuma hizo. Nalipeleka pia suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, halafu kama ni kutajwa (wabunge hao), basi tutapata mwongozo wa kamati hiyo." alisema Spika Makinda na kuongeza:
"Nasema kwa dhati kabisa, kitendo hiki hakikubaliki ndani ya Bunge hili. Wabunge mkae vizuri. Kama kuna baadhi yetu wanaenda huku na huku kujitafutia masilahi binafsi, tutawezaje kuisimamia Serikali?"
Mbunge Zedi
Baada ya Spika kutangaza kuvunja Kamati ya Nishati na Madini, Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Seleman Zedi alisema kuwa ameshtushwa na uamuzi huo na anasubiri uamuzi wa Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge.
"Nimeshtushwa sana na uamuzi huo, lakini tusubiri Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge," alisema Zedi.
Waziri Muhongo
Akihitimisha hoja ya wizara yake bungeni jana, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kuwa baadhi ya wabunge ambao wanashiriki kwenye vikao vya uamuzi vya Tanesco kama wajumbe, wamekuwa wakilihujumu shirika hilo kwa njia mbalimbali ikiwamo kufanya nalo biashara.
"Shirika liliwahi kulipa Pauni za Uingereza 50,000 kwa ajili ya kununua vipuri, lakini kilicholetwa nchini ni masanduku ya misumari,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza;
“Hata katika nguzo za umeme kuna biashara inaendelea. Tunajua kuwa nguzo hizo zinazalishwa Iringa na kupelekwa Mombasa kisha kurudishwa nchini kwa maelezo kwamba zimetoka Afrika Kusini."
Waziri Muhongo alisema kuwa mbali na ufisadi huo, baadhi ya wabunge ambao ni wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini wamewahi kuliuzia shirika hilo matairi ya magari kwa bei kubwa, bidhaa ambayo hata hivyo alisema haina ubora unaokubalika.
"Baadhi ya wabunge wanafanya biashara na Tanesco; niseme tu kuwa, hii siyo sahihi. Lakini niombe kwamba mjadala huu tuufunge kwa sababu, tayari tumekabidhi suala hilo kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)" alisema Waziri Muhongo.
Waziri Muhongo pia alizungumzia jinsi baadhi ya watu na kampuni zinavyoiibia Tanesco kupitia mita za Luku ambapo aliwataja watu hao kuwa ni pamoja na Shule za St. Mary's zinazodaiwa Sh10.5 milioni, Access Bank, Tawi la Tabata Matumbi Sh13.8 milioni na Hoteli ya Akudo Paradaise ya Kariakoo inayodaiwa Sh25.5 milioni.
Alisema kuwa baada ya kubainika kwa wadaiwa hao hutumia umeme kinyume na utaratibu,wahusika wote walikamatwa na kufikishwa kituo cha polisi baada ya kufanyika kwa uchunguzi.
“Baada ya kufanya uchunguzi na kubaini kuwapo kwa watu wanaotumia umeme bila kulipia na kuisababishia Tanesco hasara, tumeamua kuwachukulia hatua ikiwamo kuwafikisha polisi,” alisema Profesa Muhongo na kuongeza:
“Inaonyesha wazi kwamba wizi wa umeme wa Luku umekuwa ukifanyika mara kwa mara na kwamba baada ya kuwakamata hawa, uchunguzi utaendelea na wengine watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.”
Jenista Mhagama
Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama alisema kuwa, amepokea kwa masikitiko taarifa hizo za wabunge wa CCM kuingia katika tuhuma hizo, lakini akasema namna nzuri ya kushughulikia tatizo hilo ni vyombo vya dola kufanya uchunguzi makini ili kujiridhisha na kisha hatua za kisheria kufuatwa.
"Ni taarifa mbaya kwa kweli, lakini mimi niiombe Serikali itusaidie kufanya uchunguzi ili ukweli ubainike na hatua zichukuliwe," alisema Mhagama.
Mbunge Silinde
Naye Katibu wa Wabunge wa Chadema, David Silinde alisema: "Kwa kuwa tumesikia, kama kambi tutafanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo. Tutakaa kikao cha kuamua nini cha kufanya. Pia tutatoa tamko juu ya mwenendo mzima wa hizi tuhuma na Bunge kwa ujumla.”
Zitto
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Mashirika ya Umma ambayo imeunganishwa kwenye tuhuma hizo, Zitto Kabwe, alisema tuhuma hizo anazisikia, lakini anaziona kama siasa za majitaka kwa sababu zinarushwa bila ushahidi wowote.
"Hakuna hata mbunge mmoja aliyesimama kusema nani amehongwa nini. Mimi binafsi sijahongwa na mtu yeyote wala mimi sijamtetea mtu isipokuwa natetea taratibu kufuatwa," alisema.
Zitto alibainisha kuwa anaamini tuhuma hizo zimetokana na hasira za yeye kupinga posho za wabunge na sasa wameona hilo ndilo eneo la kumkomoa.
"Kwa kuwa ‘my conscious is clear’, (dhamira yangu safi) sina mashaka, uzushi, uongo na siasa za majitaka hizi zitaumbuliwa na ukweli. Hata hivyo, kwa kuwa tuhuma hizo zinasemwa juu juu tu, tutataka vyombo vya dola vichunguze na ikithibitika hatua zichukuliwe," alisema na kuongeza:
"Kwangu mimi naona hizi ni siasa za urais na hasira za posho. Wenye kutaka urais wa vyama vyote na wapambe wao, wameungana kunichafulia heshima yangu. Wabunge wenye njaa ya posho, wameungana kunikomoa. Ukweli una tabia ya kutopenda kupuuzwa. Mwalimu Nyerere (Julius) alisema katika andiko lake la 'Tujisahihishe'.”
Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini(Chadema) alishauri pia Spika wa Bunge kutumia Kamati ya Maadili kuchunguza tuhuma hizo kwa kuwa hazipaswi kuachwa zikapita hivihivi.
John Cheyo
Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali, John Cheyo alisema anasikitika kuona Bunge ambalo kimsingi ni kitovu cha uadilifu limeanza kuvamiwa na mafisadi.
"Very unfortunate, (bahati mbaya sana) Bunge ambalo ni kilele cha uadilifu, nyumba ya waheshimiwa, ambako kunatarajiwa high level of intergrity (uadilifu wa hali ya juu), kuanza kutumika kama perpets (vibaraka) wa mafisadi," alisema.
Cheyo aliongeza: "Ninalaani sana kitendo hicho, lakini niwaambie viongozi wapya wa Wizara ya Nishati na Madini kuwa, waendelee kufanya kazi kwa uadilifu na nguvu yao ni wabunge wengi wema, ambao watawaunga mkono. Wasikate tama," alisema.
Mjadala ya wabunge
Mbunge wa Maswa Magharibi (Chadema), John Shibuda aliliomba Bunge kufanya uchunguzi ili kuwabaini wabunge wanaojihusisha na vitendo vya rushwa.
Alisema baadhi ya wabunge wanatumia nafasi zao vibaya kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa ili kuiyumbisha Serikali.
“Namwomba Spika na timu yake yote ikaona kuna haja ya kufanya uchunguzi kwa wabunge ili kuweza kuwabaini wanaotumia nafasi zao vibaya kwa kujihusisha na vitendo vya rushwa ilikuiyumbisha Serikali ,” alisema Shibuda
Mbuge Kangi
Naye Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora alitaka Waziri wa Nishati na Madini awataje wabunge aliowatuhumu ili kuonyesha usawa hasa baada ya kuwataja kwa majina watuhumiwa wengine katika ufisadi wa Tanesco na wale wanaoliibia umeme shirika hilo la umma.
"Tunaomba waziri asema kwa nini asiwataje hao wengine wakati tayari ametutajia kina Freddy na Veronica William Mhando na taasisi za St Mary? " alihoji.
Hoja hiyo ya Lugora ilitupwa na Spika wa Bunge Anne Makinda aliyesema kuwa jambo hilo lina taratibu zake.
Kamata
Vicky Kimata (Viti Maalumu) nusura amwage machozi bungeni juzi jioni, alipozungumza kwa uchungu kupinga hatua ya wabunge hao kujihusisha na ufisadi, huku akieleza kuwa nchi imefika pabaya.
'Watanzania tumefikia hapo! Watu wanatengeneza mgawo wa umeme ili kujipatia hela, Jamani...jamani.. Hammwogopi hata Mungu!"
Said Mussa Zuberi alipendekeza itungwe sheria ya kuwanyonga mafisadi na wahujumu uchumi kwa kuwa matendo hayo pia ni uuaji.
"Katika taifa letu tuna wadudu sijui tuwaite mchwa ambao wanaharibu yaliyotengenezwa kwa maslahi yao. Nawashauri wananchi kwa kuwa sasa tuko kwenye suala la Katiba, wasisahau kupitisha sheria ili watu wahujumu uchumi tuwaue, tena kwa risasi.
Monday, July 23, 2012
Dar Talk" Video ya Utupu ya Agness Masogange yavuja Mtandaoni......
BAADA ya kuandamwa na skendo kibao za kutoka na vigogo kisura wa video za wasanii wa bongo,Agnes Gerald maarufu kama Agnes Masogange, ameonekana kwenye mkanda wa picha ya ngono ambao umesambaa mtaani huku ikiwa dili kwa watu wanaotaka kuona umbo la mwanadada huyo.
Mkanda huo unaomuonesha mwanadada huyo akiwa mtupu, huku utata mkubwa ukizunguka kujua ni kitu gani kilichosababisha hadi kusambazwa kwa video hiyo.
Agnes katika pozi
Mtandao wa DarTalk, ulifanikiwa kupata video hiyo ambayo mwanadada huyo ameonekana na kijana mmoja ambaye bado hajafahamika jina lake. Baadhi ya videos za bongo flava ambazo amewahi kuong’aa ni pamoja na ‘Magube gube’ ya Barnaba , Masogange ya Belle9 na nyingine nyingi.
Baada ya kupatatikana kwa video hiyo mtandao huu ulijaribu kumsaka Agnes ili kufafanua uwepo wake ndani ya video hiyo lakini hakuweza kupatikana kwenye simu yake ya mkononi.
Mkanda huo unaomuonesha mwanadada huyo akiwa mtupu, huku utata mkubwa ukizunguka kujua ni kitu gani kilichosababisha hadi kusambazwa kwa video hiyo.
Agnes katika pozi
Mtandao wa DarTalk, ulifanikiwa kupata video hiyo ambayo mwanadada huyo ameonekana na kijana mmoja ambaye bado hajafahamika jina lake. Baadhi ya videos za bongo flava ambazo amewahi kuong’aa ni pamoja na ‘Magube gube’ ya Barnaba , Masogange ya Belle9 na nyingine nyingi.
Baada ya kupatatikana kwa video hiyo mtandao huu ulijaribu kumsaka Agnes ili kufafanua uwepo wake ndani ya video hiyo lakini hakuweza kupatikana kwenye simu yake ya mkononi.
Watanzania 100 wafungwa China.....................
UKAHABA na usafirishaji wa dawa za kulevya unaofanywa na baadhi ya Watanzania ni moja ya dosari zinazotia doa uhusiano kati ya Tanzania na China.
Watanzania zaidi ya 100 wako kwenye magereza ya China wakitumikia vifungo kwa makosa ya kukutwa na dawa za kulevya, huku wasichana wanane wakirejeshwa nyumbani siku chache zilizopita kutokana na ukahaba.
Balozi wa Tanzania nchini China, Philip Marmo alibainisha hayo mwishoni mwa wiki iliyopita katika mkutano uliofanyika nyumbani kwake jijini hapa.
Mkutano huo uliambatana na chakula cha mchana, ukiwa ni maalumu kwa ajili ya Watanzania waliokuwa wakihudhuria Mkutano wa Tano wa Mawaziri wa Ushirikiano kati ya China na Tanzania (FOCAC) uliofanyika Alhamisi na Ijumaa wiki iliyopita.
Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, John Haule na wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Balozi Herbert Mhango.
Aidha, walikuwapo watendaji wakuu kadhaa wa mashirika ya umma, taasisi za umma, sekta binafsi na wafanyabiashara wa Tanzania. Balozi Marmo alisema Tanzania inajivunia uhusiano wa muda mrefu na China tangu miaka ya sitini, ilipofungua ubalozi wake Aprili 26, 1964, lakini katika siku za karibuni umekumbwa na dosari hizo mbili. “Kwa kweli hili la dawa za kulevya, linaumiza vichwa sana.
Hapa ukiwa na dawa za kulevya hufiki popote, wako makini sana. Ukikamatwa hakuna msamaha, adhabu kubwa ni kifo, kwao ni kosa kubwa,” alisema.
Balozi Marmo aliongeza: “Dawa za kulevya kwao ni suala la usalama wa Taifa, ni vigumu kuanzisha mjadala katika suala hili. Katika siku za karibuni, kumekuwa na ongezeko la vijana wetu wanaoshughulika na mihadarati.”
Alisema cha kushangaza vijana hao wanapokamatwa, pasipoti zao huonesha kuwa hawatoki Dar es Salaam, bali katika miji mingine duniani.
“Halafu si kwamba hawa wanaokamatwa wanatoka Dar es Salaam, hapana … utakuta wanatoka Istanbul, Ankara, Rio de Janeiro, Pakistani; baadaye, ndio unajua wanasema tunatoka Kinondoni, Magomeni Mapipa, Tanga, Zanzibar na Kigoma,” aliongeza Balozi.
“Hivi sasa wako Watanzania zaidi ya 100 katika jela za China. Masikini wanatumiwa tu, wengine na wafanyabiashara wakubwa tu, wengine watoto wa wakubwa,” alibainisha zaidi Balozi Marmo. Alisema dosari nyingine katika siku za karibuni, ni wasichana kutoka Tanzania kujihusisha na biashara ya ukahaba China.
“Kuna hili la wanawake wetu kujihusisha na ukahaba … hapa haikubaliki, tayari wapo wanane wanarudishwa nyumbani, wamepewa siku nane za hifadhi kabla ya kuondoka,” alisema Balozi Marmo. “Wenyeji wanatuheshimu, wenzao wa Kenya na Uganda wamepewa siku tatu tu. Kwa kweli, hali hii inaharibu uhusiano wetu mzuri na China.”
Alisema Wachina wanaipenda sana Tanzania na wanaiona Tanzania kuwa sehemu nzuri ya kuwekeza na kufanya biashara, hivyo ni vyema fursa hiyo ikatumiwa vizuri badala ya kuchafua jina la nchi.
Alikerwa pia na alichoeleza kuwa ni biashara ndogo zinazofanywa na Watanzania, hasa wanawake kwa kubeba mabegi, badala ya kuchangamkia biashara kubwa na wenzao wa Taifa hili la Asia.
“Biashara tunazofanya ni ndogo sana, akinamama wanabeba mabegi tu, hii si biashara. Tulipaswa kufanya biashara ya makontena kupeleka nyumbani,” alieleza Balozi Marmo ambaye yuko Beijing takriban miezi mitatu sasa tangu ateuliwe kushika wadhifa huo.
Balozi Marmo aliwataka Watanzania kutumia urafiki na uhusiano mzuri kati ya Tanzania na China kufanya biashara kwa manufaa yao na Taifa. Mwito huo uliungwa mkono na mawaziri Membe na Teu ambao waliwataka wafanyabiashara hao na Watanzania kwa jumla, kuchangamkia fursa zinazopatikana China.
Katika miaka ya karibuni, China imekuwa mshirika mpya wa mataifa ya Afrika katika maendeleo, na imekuwa ikifadhili miradi mingi kuanzia elimu hadi masuala ya michezo na utamaduni.
Watanzania zaidi ya 100 wako kwenye magereza ya China wakitumikia vifungo kwa makosa ya kukutwa na dawa za kulevya, huku wasichana wanane wakirejeshwa nyumbani siku chache zilizopita kutokana na ukahaba.
Balozi wa Tanzania nchini China, Philip Marmo alibainisha hayo mwishoni mwa wiki iliyopita katika mkutano uliofanyika nyumbani kwake jijini hapa.
Mkutano huo uliambatana na chakula cha mchana, ukiwa ni maalumu kwa ajili ya Watanzania waliokuwa wakihudhuria Mkutano wa Tano wa Mawaziri wa Ushirikiano kati ya China na Tanzania (FOCAC) uliofanyika Alhamisi na Ijumaa wiki iliyopita.
Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, John Haule na wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Balozi Herbert Mhango.
Aidha, walikuwapo watendaji wakuu kadhaa wa mashirika ya umma, taasisi za umma, sekta binafsi na wafanyabiashara wa Tanzania. Balozi Marmo alisema Tanzania inajivunia uhusiano wa muda mrefu na China tangu miaka ya sitini, ilipofungua ubalozi wake Aprili 26, 1964, lakini katika siku za karibuni umekumbwa na dosari hizo mbili. “Kwa kweli hili la dawa za kulevya, linaumiza vichwa sana.
Hapa ukiwa na dawa za kulevya hufiki popote, wako makini sana. Ukikamatwa hakuna msamaha, adhabu kubwa ni kifo, kwao ni kosa kubwa,” alisema.
Balozi Marmo aliongeza: “Dawa za kulevya kwao ni suala la usalama wa Taifa, ni vigumu kuanzisha mjadala katika suala hili. Katika siku za karibuni, kumekuwa na ongezeko la vijana wetu wanaoshughulika na mihadarati.”
Alisema cha kushangaza vijana hao wanapokamatwa, pasipoti zao huonesha kuwa hawatoki Dar es Salaam, bali katika miji mingine duniani.
“Halafu si kwamba hawa wanaokamatwa wanatoka Dar es Salaam, hapana … utakuta wanatoka Istanbul, Ankara, Rio de Janeiro, Pakistani; baadaye, ndio unajua wanasema tunatoka Kinondoni, Magomeni Mapipa, Tanga, Zanzibar na Kigoma,” aliongeza Balozi.
“Hivi sasa wako Watanzania zaidi ya 100 katika jela za China. Masikini wanatumiwa tu, wengine na wafanyabiashara wakubwa tu, wengine watoto wa wakubwa,” alibainisha zaidi Balozi Marmo. Alisema dosari nyingine katika siku za karibuni, ni wasichana kutoka Tanzania kujihusisha na biashara ya ukahaba China.
“Kuna hili la wanawake wetu kujihusisha na ukahaba … hapa haikubaliki, tayari wapo wanane wanarudishwa nyumbani, wamepewa siku nane za hifadhi kabla ya kuondoka,” alisema Balozi Marmo. “Wenyeji wanatuheshimu, wenzao wa Kenya na Uganda wamepewa siku tatu tu. Kwa kweli, hali hii inaharibu uhusiano wetu mzuri na China.”
Alisema Wachina wanaipenda sana Tanzania na wanaiona Tanzania kuwa sehemu nzuri ya kuwekeza na kufanya biashara, hivyo ni vyema fursa hiyo ikatumiwa vizuri badala ya kuchafua jina la nchi.
Alikerwa pia na alichoeleza kuwa ni biashara ndogo zinazofanywa na Watanzania, hasa wanawake kwa kubeba mabegi, badala ya kuchangamkia biashara kubwa na wenzao wa Taifa hili la Asia.
“Biashara tunazofanya ni ndogo sana, akinamama wanabeba mabegi tu, hii si biashara. Tulipaswa kufanya biashara ya makontena kupeleka nyumbani,” alieleza Balozi Marmo ambaye yuko Beijing takriban miezi mitatu sasa tangu ateuliwe kushika wadhifa huo.
Balozi Marmo aliwataka Watanzania kutumia urafiki na uhusiano mzuri kati ya Tanzania na China kufanya biashara kwa manufaa yao na Taifa. Mwito huo uliungwa mkono na mawaziri Membe na Teu ambao waliwataka wafanyabiashara hao na Watanzania kwa jumla, kuchangamkia fursa zinazopatikana China.
Katika miaka ya karibuni, China imekuwa mshirika mpya wa mataifa ya Afrika katika maendeleo, na imekuwa ikifadhili miradi mingi kuanzia elimu hadi masuala ya michezo na utamaduni.
Monday, July 2, 2012
Gari La Jackline Wolper Lakamatwa...........
LILE gari la kifahari aina ya BMW X6 lenye namba za usajili T 574 BXF linalomilikiwa na staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper Masawe limedakwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Kwa mujibu wa ofisa mmoja wa TRA ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, gari hilo la kisasa lilikamatwa Juni 28, 2012 kupitia Kampuni ya Mnada ya Majembe kutokana na sababu kadha wa kadha.
SABABU ZAANIKWA
Akiendelea kufunguka, afisa huyo alisema kuwa sababu ya kwanza ni kuhisiwa kuwa gari hilo liliingizwa nchini kinyemela kutokana na vielelezo vyake vya kwenye kadi kupitia kwenye vyombo vya habari, ndipo taa nyekundu ikawaka ndani ya vichwa vya maafisa wa TRA na kuanza kulifuatilia.
Alidai kuwa mbali ya kuingia nchini kinyemela, lakini BMW hilo halijalipiwa ushuru zaidi ya miaka mitano iliyopita kwa mujibu wa vielelezo vyake.
MPANGO WA KULIKAMATA ULIVYOSUKWA
Kwa mujibu wa ofisa huyo, ili kufanikisha zoezi la kulikamata gari hilo, vijana kutoka kampuni ya Majembe waliingia mzigoni kulisaka ambapo kuna mtu alipiga kambi jirani na makazi ya Wolper, Mbezi Beach jijini Dar.
Ilisemekana kuwa vijana hao walikuwa na kazi moja tu, kuhakikisha anapotoka Jack wanamfuatilia hatua kwa hatua hadi mahali atakapokwenda kupiga kambi na kulitia mikononi.
“Haikuwa kazi rahisi maana muda mrefu alikuwa haonekani nalo, ndipo mpango huo ulipokuja kukamilishwa kwa njia ya kumfuatilia anapotoka kwake hadi mahali lilipokamatwa maeneo ya katikati ya Jiji la Dar,” alisema.
Akaendelea kudai: “Unajua hawa mastaa wetu kuna vitu wanavifanya bila kujua madhara yake, kitendo cha Wolper kuonesha kadi ya gari kwa waandishi wa habari huku anafahamu ina mapungufu kibao ndiyo sababu kuu ya gari hilo kuanza kufuatiliwa.”
MH! ETI USHURU MILIONI 70?
Taarifa nyingine ya kushtua ni kwamba ilidaiwa kuwa kuwa TRA peke yake inadai Sh. milioni 70 za ushuru.
“Si fedha ndogo zinazodaiwa na TRA, kwa hesabu ya harakaharaka ni zaidi ya Sh. milioni 70 ambazo zinatakiwa kulipwa.”
Baada ya The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda kujiridhisha kuwa gari hilo limedakwa, lilimuendea hewani Wolper lakini hakuweza kupokea simu hadi gazeti linakwenda mitamboni.
Kwa mujibu wa ofisa mmoja wa TRA ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, gari hilo la kisasa lilikamatwa Juni 28, 2012 kupitia Kampuni ya Mnada ya Majembe kutokana na sababu kadha wa kadha.
SABABU ZAANIKWA
Akiendelea kufunguka, afisa huyo alisema kuwa sababu ya kwanza ni kuhisiwa kuwa gari hilo liliingizwa nchini kinyemela kutokana na vielelezo vyake vya kwenye kadi kupitia kwenye vyombo vya habari, ndipo taa nyekundu ikawaka ndani ya vichwa vya maafisa wa TRA na kuanza kulifuatilia.
Alidai kuwa mbali ya kuingia nchini kinyemela, lakini BMW hilo halijalipiwa ushuru zaidi ya miaka mitano iliyopita kwa mujibu wa vielelezo vyake.
MPANGO WA KULIKAMATA ULIVYOSUKWA
Kwa mujibu wa ofisa huyo, ili kufanikisha zoezi la kulikamata gari hilo, vijana kutoka kampuni ya Majembe waliingia mzigoni kulisaka ambapo kuna mtu alipiga kambi jirani na makazi ya Wolper, Mbezi Beach jijini Dar.
Ilisemekana kuwa vijana hao walikuwa na kazi moja tu, kuhakikisha anapotoka Jack wanamfuatilia hatua kwa hatua hadi mahali atakapokwenda kupiga kambi na kulitia mikononi.
“Haikuwa kazi rahisi maana muda mrefu alikuwa haonekani nalo, ndipo mpango huo ulipokuja kukamilishwa kwa njia ya kumfuatilia anapotoka kwake hadi mahali lilipokamatwa maeneo ya katikati ya Jiji la Dar,” alisema.
Akaendelea kudai: “Unajua hawa mastaa wetu kuna vitu wanavifanya bila kujua madhara yake, kitendo cha Wolper kuonesha kadi ya gari kwa waandishi wa habari huku anafahamu ina mapungufu kibao ndiyo sababu kuu ya gari hilo kuanza kufuatiliwa.”
MH! ETI USHURU MILIONI 70?
Taarifa nyingine ya kushtua ni kwamba ilidaiwa kuwa kuwa TRA peke yake inadai Sh. milioni 70 za ushuru.
“Si fedha ndogo zinazodaiwa na TRA, kwa hesabu ya harakaharaka ni zaidi ya Sh. milioni 70 ambazo zinatakiwa kulipwa.”
Baada ya The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda kujiridhisha kuwa gari hilo limedakwa, lilimuendea hewani Wolper lakini hakuweza kupokea simu hadi gazeti linakwenda mitamboni.
Subscribe to:
Posts (Atom)


















