Sunday, May 27, 2012

Uwoya, Patcho(tajiri) Wapeleka Arobaini ya Kanumba Congo

Patcho Mwamba.
Na Shakoor Jongo
MASTAA wanaotamba katika filamu za Kibongo, Irene Pancras Uwoya na Patcho Mwamba ‘Tajiri’ Mei 23, mwaka huu wameupeleka msiba wa staa mwenzao, marehemu Steven Kanumba huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa ajili ya maombolezo.
Wakizungumza na Ijumaa muda mchache kabla ya kukwea pipa, mastaa hao walisema wamepewa mwaliko na baadhi ya wafanyabiashara wa nchini humo kwa ajili ya kwenda kumalizia msiba wa Kanumba.
“Unajua kifo cha Kanumba kimewagusa watu wengi, siyo Watanzania tu, hata kule kwetu pia kulikuwa na maombolezo, kwa kuwa arobaini imeshapita wametupa mwaliko kwenda kujumuika nao,” alisema Patcho ambaye pia ni mwanamuziki wa Bendi ya FM Academia.
Mei 17, mwaka huu, Kanumba alitimiza siku 40 tangu alipofariki na shughuli za kumalizia msiba zilifanyika jijini Dar kwa baadhi ya ndugu zake na mastaa kutembelea kaburi lake na kituo cha watoto yatima cha Kuwama

No comments:

Post a Comment